logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchezaji wa Roma kuichukua hatua za kisheria klabu hiyo kwa kumtishia maisha

Familia ya Zaniola ilisema kuwa mashabiki waliojawa na hasira walifika kwake.

image
na Radio Jambo

Makala02 February 2023 - 06:44

Muhtasari


• Mchezaji huyo wa Kiitaliano alikuwa karibu na kuondoka kwenye Serie A baada ya kikosi cha Jose Mourinho kufikia makubaliano ya pauni milioni 30 na Bournemouth wiki iliyopita.

Nicvolo Zaniola wa Roma kuishtaki klabu hiyo kwa kumtishia maisha

Nicolo Zaniolo, Winga wa timu ya AS Roma inayoshiriki katika ligi ya Italia Serie A ana mpango wa kuwashtaki Roma kwa 'shinikizo la kisaikolojia na kuwashawishi' katika kipindi chote cha uhamisho wa Januari, kulingana na ripoti.

Inadaiwa kwamba Zaniola alipokea vitisho vya maisha kutoka kwa watu ndani ya klabu hiyo wakiwemo mashabiki baada ya kukataa kuuzwa katika kipindi cha dirisha la uhamisho Januari.

Mchezaji huyo wa Kiitaliano alikuwa karibu na kuondoka kwenye Serie A baada ya kikosi cha Jose Mourinho kufikia makubaliano ya pauni milioni 30 na Bournemouth wiki iliyopita.

Awali Zaniolo alikataa hatua hiyo lakini alionekana kubadili mawazo yake siku moja baadaye, hata hivyo Cherries ndio ambao hatimaye walirudi nyuma kwenye mpango huo kutokana na matatizo ya kifedha, Daily Mail Walisema.

Familia ya Zaniolo inadai kwamba 'matamshi ya hivi majuzi ya vyombo vya habari' dhidi ya Muitaliano huyo yamechochewa na klabu.

“Baada ya habari kusambaa kuhusu tamaa ya Zaniolo kuondoka klabuni hapo kwenye dirisha la usajili la Januari, winga huyo alipokea vitisho vya kuuawa na kulazimika kupiga simu polisi baada ya mashabiki wa Roma waliokuwa na hasira kujitokeza nyumbani kwake,” Mail walisema.

Klabu hiyo ilimpa ruhusa ya kusafiri hadi La Spezia na familia yake kwa saa 48 wakati mazungumzo yakiendelea.

Pia wanaripoti kuwa timu ya mawakili wamewasiliana kushughulikia suala hilo. Assocalciatori, ambao wana jukumu la kusaidia wachezaji katika migogoro na vilabu vyao, pia wamearifiwa.

Inaeleweka kuwa Zaniolo atamsubiri Tiago Pinto - mkurugenzi wa michezo wa Roma - kuhudhuria mkutano wake na waandishi wa habari ulioratibiwa kabla ya kutoa maoni juu ya hali hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved