Mamake Rais wa FA wa Uhispania asusia kula kwa sababu ya mzozo ‘kupigana busu’

Rubiales aliapa kutojiuzulu Ijumaa lakini alisimamishwa kazi na shirikisho la soka duniani Fifa siku ya Jumamosi.

Muhtasari
  • Hermoso, 33, alisema hakukubali busu wakati wa hafla ya uwasilishaji wa taji huko Sydney mnamo Agosti 20 .
Rais wa FA Uhispania akosolewa kwa kumpiga busu mchezaji
Image: BBC

Mamake rais wa shirikisho la soka la Uhispania Luis Rubiales amegoma kula kwa sababu ya "windaji wenye hila " dhidi ya mwanawe.

Kumekuwa na ukosoaji mkubwa dhidi ya Rubiales, 46, baada ya kumbusu fowadi Jenni Hermoso kwenye midomo kufuatia ushindi wa fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake wa timu ya Uhispania.

Mama yake, Angeles Bejar, sasa amejifungia katika kanisa moja huko Motril.

Aliliambia shirika la habari la Uhispania EFE kuwa mgomo wake utaendelea "kwa muda usiojulikana, mchana na usiku".

Hermoso, 33, alisema hakukubali busu wakati wa hafla ya uwasilishaji wa taji huko Sydney mnamo Agosti 20 .

Rubiales aliapa kutojiuzulu Ijumaa lakini alisimamishwa kazi na shirikisho la soka duniani Fifa siku ya Jumamosi.

Vyombo vya habari vya Uhispania vimekusanyika nje ya kanisa la Divina Pastora huko Motril kwenye pwani ya kusini ya Uhispania, mji ambao Rubiales alilelewa.

Bejar aliiambia EFE kwamba "uwindaji wa kinyama na wa umwagaji damu ambao anafanyiwa na mwanangu ni jambo ambalo hastahili".