Majina ya wanasoka mahiri walioteuliwa kuwania tuzo ya heshima zaidi katika soka, Ballon d’Or yalitangazwa siku ya Jumatano jioni.
Jarida la France Football Magazine lilitangaza orodha ya wachezaji 30 walioteuliwa kuwania tuzo hiyo kabla ya hafla kuu ya tuzo itakayofanyika kwenye ukumbi wa Theatre Chatelet jijini Paris, Ufaransa mnamo Oktoba 30.
Mshindi wa Kombe la Dunia 2022 na Ligue 1 2022/23 Lionel Messi ni miongoni mwa wachezaji walioteuliwa. Katika orodha hiyo pia walikuwemo washambuliaji matata Kylian Mbappe wa PSG na timu ya taifa ya Ufaransa, Erling Halaand wa Manchester City na Norway, Mohammed Salah wa Liverpool na Misri, Bukayo Saka wa Arsenal na Uingereza, miongoni mwa wengine. Mshambulizi Christiano Ronaldo, ambaye sasa anachezea Al Nassr ya Saudi Arabia, hakufaulu kwenye orodha hiyo kwa mara ya kwanza tangu 2003.
Lionel Messi, Erling Halaand na Kylian Mbapppe ni miongoni mwa wanaotajwa sana kushinda tuzo hiyo. Iwapo Messi atashinda tena tuzo hiyo ya kifahari, itakuwa ni mara yake ya nane kuipeleka nyumbani.
Tazama orodha kamili ya wateuliwa wa tuzo ya Ballon d'Or;
- André Onana - Manchester United/Cameroon
- Josko Gvardiol - Manchester City/Croatia
- Karim Benzema - Al Ittihad
- Jamal Musiala - Bayern Munich/Germany
- Mohamed Salah - Liverpool/Egypt
- Jude Bellingham - Real Madrid/England
- Bukayo Saka - Arsenal/England
- Randal Kolo Muani - Paris Saint-Germain/France
- Kevin De Bruyne - Manchester City/Belgium
- Bernardo Silva - Manchester City/Portugal
- Emiliano Martínez - Aston Villa/Argentina
- Khvicha Kvaratskhelia - Napoli/Georgia
- Rúben Dias - Manchester City/Portugal
- Nicolo Barella - Inter Milan/Italy
- Erling Haaland - Manchester City/Norway
- Yassine Bounou - Al Hilal/Morocco
- Martin Ødegaard - Arsenal/Norway
- Julián Álvarez - Manchester City/Argentina
- Ilkay Gündogan - Barcelona/Germany
- Vinícius Júnior - Real Madrid/Brazil
- Lionel Messi - Inter Miami/Argentina
- Rodri - Manchester City/Spain
- Lautaro Martínez - Inter Milan/Argentina
- Antoine Griezmann - Atletico Madrid/France
- Robert Lewandowski - Barcelona/Poland
- Kylian Mbappé - Paris Saint-Germain/France
- Kim Min-jae - Napoli/South Korea
- Victor Osimhen - Napoli/Nigeria
- Luka Modric - Real Madrid/Croatia
- Harry Kane - Bayern Munich/England