logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama orodha kamili ya wanasoka bora walioteuliwa kuwania Ballon d'Or

Lionel Messi, Erling Halaand na Kylian Mbapppe ni miongoni mwa wanaotajwa sana kushinda tuzo hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari07 September 2023 - 03:48

Muhtasari


•Wanasoka mahiri walioteuliwa kuwania tuzo ya heshima zaidi katika soka, Ballon d’Or yalitangazwa siku ya Jumatano jioni.

•Lionel Messi, Erling Halaand na Kylian Mbapppe ni miongoni mwa wanaotajwa sana kushinda tuzo hiyo. 

Messi apokea tuzo la mchezaji bora kwa mara ya 7

Majina ya wanasoka mahiri walioteuliwa kuwania tuzo ya heshima zaidi katika soka, Ballon d’Or yalitangazwa siku ya Jumatano jioni.

Jarida la France Football Magazine lilitangaza orodha ya wachezaji 30 walioteuliwa kuwania tuzo hiyo kabla ya hafla kuu ya tuzo itakayofanyika kwenye ukumbi wa Theatre Chatelet jijini Paris, Ufaransa mnamo Oktoba 30.

Mshindi wa Kombe la Dunia 2022 na Ligue 1 2022/23 Lionel Messi ni miongoni mwa wachezaji walioteuliwa. Katika orodha hiyo pia walikuwemo washambuliaji matata Kylian Mbappe wa PSG na timu ya taifa ya Ufaransa, Erling Halaand wa Manchester City na Norway, Mohammed Salah wa Liverpool na Misri, Bukayo Saka wa Arsenal na Uingereza, miongoni mwa wengine. Mshambulizi Christiano Ronaldo, ambaye sasa anachezea Al Nassr ya Saudi Arabia, hakufaulu kwenye orodha hiyo kwa mara ya kwanza tangu 2003.

Lionel Messi, Erling Halaand na Kylian Mbapppe ni miongoni mwa wanaotajwa sana kushinda tuzo hiyo. Iwapo Messi atashinda tena tuzo hiyo ya kifahari, itakuwa ni mara yake ya nane kuipeleka nyumbani.

Tazama orodha kamili ya wateuliwa  wa tuzo ya Ballon d'Or;

 

  1. André Onana - Manchester United/Cameroon
  2. Josko Gvardiol - Manchester City/Croatia
  3. Karim Benzema - Al Ittihad
  4. Jamal Musiala - Bayern Munich/Germany
  5. Mohamed Salah - Liverpool/Egypt
  6. Jude Bellingham - Real Madrid/England
  7. Bukayo Saka - Arsenal/England
  8. Randal Kolo Muani - Paris Saint-Germain/France
  9. Kevin De Bruyne - Manchester City/Belgium
  10. Bernardo Silva - Manchester City/Portugal
  11. Emiliano Martínez - Aston Villa/Argentina
  12. Khvicha Kvaratskhelia - Napoli/Georgia
  13. Rúben Dias - Manchester City/Portugal
  14. Nicolo Barella - Inter Milan/Italy
  15. Erling Haaland - Manchester City/Norway
  16. Yassine Bounou - Al Hilal/Morocco
  17. Martin Ødegaard - Arsenal/Norway
  18. Julián Álvarez - Manchester City/Argentina
  19. Ilkay Gündogan - Barcelona/Germany
  20. Vinícius Júnior - Real Madrid/Brazil
  21. Lionel Messi - Inter Miami/Argentina
  22. Rodri - Manchester City/Spain
  23. Lautaro Martínez - Inter Milan/Argentina
  24. Antoine Griezmann - Atletico Madrid/France
  25. Robert Lewandowski - Barcelona/Poland
  26. Kylian Mbappé - Paris Saint-Germain/France
  27. Kim Min-jae - Napoli/South Korea
  28. Victor Osimhen - Napoli/Nigeria
  29. Luka Modric - Real Madrid/Croatia
  30. Harry Kane - Bayern Munich/England

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved