England yaweza tu kupiga Ureno kupitia 'PS5', si kwa mchezo halisi - Bruno Fernandes atania

Ureno wanaweza tu kutana na Uingereza kwenye fainali ya Euro 2024 ikiwa timu zote mbili zitatinga kwenye fainali ya Euro

Muhtasari

• Bruno Fernandes ametania kuwa Uingereza yaweza tu kushinda Ureno kupitia ulimwengu wa mtandaoni wa soka wa PlayStation[PS] kupitia chaneli ya YouTube ya Pro Direct Soccer.

• Ureno watakuwa wanacheza hii leo Julai 1 dhidi ya Slovenia ili kujihakikishia nafasi kwenye nane bora katika kombe la  Euro  2024.

Bruno Fernandes
Image: Facebook

Kiungo wa Ureno,Bruno Fernandes amekejeli kwa ucheshi matarajio ya Uingereza ya Euro 2024, akitania kwamba njia pekee ambayo taifa hilo linaweza kuishinda Ureno ni katika ulimwengu wa mtandaoni wa PlayStation.

Ureno itamenyana na Slovenia Jumatatu usiku kwa kujiamini kwa hali ya juu, ikiwa imefuzu hatua ya makundi ya Euro 2024 kwa kushinda mara mbili na kushindwa moja.

Nayo Uingereza tayari wametinga hatua ya nane ya mwisho baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Slovakia bila suluhu. Hii ni baada ya magoli kutoka kwa Harry Kane na Jude Bellingham.

Pamoja na mchezaji mwenzake wa kimataifa Ruben Dias, nahodha wa Manchester United Fernandes alichukua fursa hiyo kuwakejeli vijana wa Gareth Southgate wiki hii wakati wa mchezo wa EA Sports FC 24.

"Kitu pekee ninachopaswa kusema ni kwamba hii ndiyo nafasi pekee ambayo England ina nafasi ya kushinda Ureno - kwenye PlayStation," Fernandes alisema kwenye chaneli ya You tube ya Pro Direct Soccer.

Kikosi cha Roberto Martinez kiliishinda Czechia 2-1 katika mchezo wao wa kwanza wa michuano ya Ulaya mwaka huu, kabla ya kuilaza Uturuki 3-0, huku Fernandes akifunga bao pekee.

Ureno ilishindwa 2-0 na Georgia katika mechi yao ya mwisho ya kundi F lakini kufuzu ilikuwa tayari imethibitishwa.

Watamenyana na Slovenia siku ya Jumatatu wakitaka kutinga hatua ya robo fainali, ambapo watamenyana na Ufaransa au Ubelgiji ikiwa wanaweza kujihakikishia nafasi yao.

Wakiwa wamepangwa upande wa pili wa mabano na Uingereza, Uingereza watapata tu nafasi ya kuthibitisha Fernandes amekosea ikiwa pande zote mbili zinaweza kutinga fainali ya Euro 2024.