Kwa nini Chelsea inaendelea kumlipa kocha Graham Potter £200k kwa wiki hadi Oktoba

Kocha huyo alifutwa na Chelsea mnamo Aprili 2 mwaka uliopita na imebainika kwamba mpaka sasa, Chelsea wamekuwa wakimlipa pauni laki 2 kila wiki na wataendelea umlipa hivyo hadi Oktoba mwaka huu.

Muhtasari

• Hata hivyo, mkufunzi  huyo mwenye umri wa miaka 49 hakuweza kubadilisha fujo iliyokuwa ndani ya timu ya Chelsea na hatimaye alifutwa kazi baada ya miezi sita pekee.

 

Graham Potter
Image: HISANI

Mnamo Aprili 2023, Chelsea ilimtimua Graham Potter miezi michache tu baada ya kukaa Stamford Bridge na kama ilivyofichuliwa na jarida la Caught Offside, The Blues bado wanamlipa kocha huyo wa Uingereza pauni 200,000 kwa wiki.

Kocha huyo wa zamani wa Brighton alipewa nafasi ya kuchukua miamba hao wa Ligi Kuu ya Uingereza Septemba 2022 baada ya kutimuliwa kwa Thomas Tuchel, huku Potter akisaini mkataba wa miaka mitano na timu hiyo ya London Magharibi.

Hata hivyo, mkufunzi  huyo mwenye umri wa miaka 49 hakuweza kubadilisha fujo iliyokuwa ndani ya timu ya Chelsea na hatimaye alifutwa kazi baada ya miezi sita pekee.

Kulingana na Mike Keegan wa The Daily Mail, klabu hiyo ya Ligi ya Premia bado inamlipa Potter mshahara wa karibu £200,000 kwa wiki, ambao utaendelea hadi Oktoba.

Kocha huyo Muingereza bado hajapata klabu mpya baada ya kutimuliwa Stamford Bridge lakini amekuwa akihusishwa na kibarua cha Uingereza kufuatia uamuzi wa Gareth Southgate kujiondoa kwenye nafasi hiyo baada ya kushindwa kwa Three Lions kwenye fainali ya Euro 2024.

Hii itakuwa fursa nzuri kwa Potter, ambaye hisa zake hazijashuka sana ukizingatia kushindwa kwa makocha wengine katika Chelsea tangu aondoke.