Je,mashabiki wa Chelsea waliudhika kuona Mount na Jorginho wakizungumza kwa furaha?

shabiki mmoja alidai kuwa anahuzuni kutazama wawili wao wakicheka

Muhtasari

•Mashabiki wa Chelsea walionyesha hisia tofauti baada ya kuona Jorginho na Mount wakicheka na kufurahia baada ya mechi kati ya Arsenal na Man-United.

•Wawili hao walikuwa Chelsea na kushinda mataji hitajika kama vile kombe la klabu bingwa Ulaya na kombe la klabu bora duniani.

Mason Mount na Jorginho wakizungumza baada ya mechi kati ya Arsenal na Manchester United.
Mason Mount na Jorginho wakizungumza baada ya mechi kati ya Arsenal na Manchester United.
Image: Facebook

Magwiji wa Chelsea,Jorginho na Mason Mount walikutana tena wakati wa mechi ya kirafiki ya Arsenal na Manchester United ya kujiandaa msimu mpya nchini Marekani.

Na hiyo ilirejesha hisia kali za shauku kwa mashabiki wa The Blues ambao walichukua safari ya kihisia chini ya kumbukumbu.

Jorginho wa Arsenal na Mount wa United walikutana Jumamosi kwenye uwanja wa SoFi huko California wakati wa ziara ya majira ya joto ya timu hizo nchini Marekani.

Viungo hao wawili walionekana wachangamfu walipokuwa na mazungumzo mazuri ya kirafiki baada ya ushindi wa The Gunners wa mabao 2-1, ambao ulifanyika muda mfupi baada ya mchezo mwingine wa kutatanisha na Chelsea ambao walifungwa 4-1 na Celtic.

Hilo lilileta hali ya huzuni kwa mashabiki wachache wa Chelsea huku wakiwakumbuka wakishinda mataji kwenye uwanja wa Stamford Bridge, kama vile ligi ya mabingwa na kombe la dunia la vilabu la Fifa, kabla ya kuondoka kwao bila kujali.

Mfuasi mmoja alitweet:

"Nina huzuni kutazama hii kwa sababu fulani.

"Mwingine alisema: "Wote wawili wanaonekana kuwa na furaha sana kaka!"

Wa tatu aliuliza: "'Je, uliona mechi ya Chelsea mapema?"

Mwingine  alisema: "Nimemkumbuka mtu wangu @mount."Mhitimu wa akademi ya Chelsea,

Mount aliondoka Stamford Bridge mnamo 2023 baada ya miaka 18 na klabu hiyo ambapo alifunga mabao 33 na kusaidia 35 katika mechi 195.

Mchezaji huyo alihamia kwa wapinzani wa  karibu ,Manchester United baada ya kuhisi kuwa hakuwa sehemu ya mipango ya wamiliki wa Chelsea.

Jorginho aliondoka Chelsea Januari 2023 baada ya miaka mitano na klabu hiyo, ambayo ilijumuisha mabao 29 na kutoa pasi nane za mabao katika mechi 213, kwa wapinzani wao Arsenal.

Kiungo huyo pia aliondoka London Magharibi kwa sababu hakuwa tena sehemu ya mipango ya kikosi cha kwanza.