Eliud Kipchoge atembelea kikosi cha Man Utd Old Trafford, apokezwa jezi na nahodha Fernandes

Kipchoge pia alishuhudia Man Utd ikigaragazwa nyumbani na Liverpool mabao 3-0 akiwa ameketi kando na CEO wa INEOS, Jim Ratcliff katika uwanja wa Old Trafford.

Muhtasari

• Awali, marathoner huyo wa Kenya alikuwa ametembelea kituo cha mazoezi cha Man Utd, Carrington ambapo alionekana akifanya mazungumzo na wachezaji.

ELIUD KIPCHOGE
ELIUD KIPCHOGE
Image: FACEBOK

Gwiji wa mbio za Marathon Eliud Kipchoge aliona ziara yake Old Trafford ikiisha kwa taabu huku wenyeji wake Manchester United wakizidiwa kabisa na wapinzani wao Liverpool.

Kipchoge alikuwa miongoni mwa mashabiki zaidi ya elfu 70 walioshuhudia pambano kati ya Man Utd na Liverpool Jumapili jioni katika uga wa Old Trafford.

Awali, marathoner huyo wa Kenya alikuwa ametembelea kituo cha mazoezi cha Man Utd, Carrington ambapo alionekana akifanya mazungumzo na wachezaji.

Ziara ya Kipchoge ilifadhiliwa na mkuu wa INEOS, Jim Ratcliffe ambaye pia ni mmiliki wa hisa ndogo katika klabu ya Man Utd.

“Kutoka Barcelona hadi Manchester. Imekuwa nzuri kutembelea timu tofauti za INEOS Sports Family. Jana tulipata fursa ya kutembelea @manchesterunited na kubadilishana ujuzi na timu ya utendaji na wachezaji,” Kipchoge alisema huku akionyesha picha akikabidhiwa jezi na nahodha Bruno Fernandes.

Luis Dias aliipa Liverpool faida ya 2-0 wakati wa mapumziko baada ya mabao mawili ya haraka huku United wakipambana na kasi na mdundo wa mechi kabla ya Mohamed Salah kupata bao lake la kawaida Old Trafford kipindi cha pili na mabao yangeweza kuwa mengi zaidi kama vijana wa Arne Slot wangechukua zao zote.

Kulikuwa na nyakati za wasiwasi kwa Ten Hag wakati Ratcliffe alionekana akishika kichwa chake mikononi mwake kwa kukata tamaa wakati mechi ikiendelea.