Mwanasoka huyu wa Kenya wengi wanamtaja kama aliyezaliwa eneo la Nairobi huku wengine wakieleza kwamba anatokea eneo la mombasa. Ila hakuna tarifa kamili kuhusu chimbuko lake.
Mohammed Bajaber, alizaliwa tarehe 15 Machi 2003, ni mchezaji ambaye kwa sasa anacheza kama kiungo mshambuliaji katika klabu ya Kenya Police FC na timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars.
Safari ya soka ya Bajaber ilianza katika akademia ya Starfield iliyopo Parklands, Nairobi. Mnamo Agosti 2021, alipata nafasi ya kwenda majaribio katika klabu ya juu ya Denmark, FC Midtjylland.
Ingawa hakusajiliwa rasmi, uzoefu huo ulimpa maarifa na motisha zaidi. Mwezi Februari 2022, alijiunga na Nairobi City Stars kwa mkataba wa mkopo wa muda mfupi kutoka Starfield Academy.
Alicheza mechi yake ya kwanza katika Ligi Kuu ya Kenya tarehe 15 Mei 2022 dhidi ya Tusker FC, na kufunga bao lake la kwanza tarehe 16 Machi 2023 dhidi ya Wazito FC.
Katika msimu wa 2023-2024, Bajaber alionyesha uwezo mkubwa, akifunga mabao sita na kutoa pasi nne za mabao, akijitambulisha kama kiungo mbunifu.
Mwezi Februari 2025, alihamia Kenya Police FC, ambapo ameanza kwa kishindo, akifunga mabao matatu katika mechi tatu za mwanzo.
Mbali na mafanikio ya klabu, Bajaber alipata mwaliko katika timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, na alicheza katika Kombe la Mapinduzi mwezi Januari 2025. Anasema uzoefu huo umemsaidia kukuza mchezo wake na kujitathmini dhidi ya wachezaji bora katika mpira wa miguu.
Kwa sasa, akiwa na umri wa miaka 22, Bajaber anaendelea kung'ara katika soka la Kenya, akionyesha matumaini ya kucheza soka la kimataifa katika siku zijazo kwa ueledi mkubwa mno.Jana alifunga goli zuri sana dhidi ya Gambia