logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Ilikuwa wakati mbaya zaidi maishani!" Ronaldo afunguka kuhusu kumpoteza mwanawe mchanga

Angél, alikufa wakati wa kuzaliwa mnamo Aprili 18, lakini pacha wake Bella alinusurika.

image
na Radio Jambo

Habari16 November 2022 - 03:56

Muhtasari


•Ronaldo alisema yeye na mkewe Georgina Rodriguez walikuwa na matumaini kwamba mtoto wao Angél angekuwa na maisha ya kawaida.

•Ronaldo alifichua kuwa ameweka majivu ya Angél karibu na yale ya baba yake, ambaye alifariki  mwaka 2005 kutokana na matatizo ya ini.

Mshambulizi wa Manchester United Christiano Ronaldo amekiri kuwa kumpoteza mtoto wake mchanga mapema mwaka huu ni moja ya matukio mabaya zaidi maishani mwake.

Katika mahojiano na mtangazaji wa Uingereza Piers Morgan, Ronaldo alisema yeye na mkewe Georgina Rodriguez walikuwa na matumaini kwamba mtoto wao Angél angekuwa na maisha ya kawaida, alikiri iliwaumiza sana mtoto huyo alipofariki mnamo siku ya kuzaliwa.

"Pengine ni kumbukumbu mbaya zaidi niliyopitia maishani tangu baba yangu alipofariki. Unajua unapokuwa na mtoto  na unatarajia kila kitu kitakuwa kawaida alafu mwishowe anakuwa na shida, ni ngumu. Georgina na mimi tulikuwa na wakati mgumu sana," alisema.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno alisema kwamba yeye na mkewe walishindwa kuelewa kabisa  kilichokuwa kikiendelea na kila mara walihoji kwa nini iliwatendekea wao. Alisema kuwa familia yake iliguswa sana na matukio hayo.

Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 37 na mkewe Georgina Rodriguez walifichua kwa huzuni kwamba mtoto wao mchanga,  Angél, alikufa wakati wa kuzaliwa mnamo Aprili 18, lakini pacha wake Bella alinusurika.

Katika mahojiano, Ronaldo alikiri kuwa alishindwa la kufanya, hakujua ikiwa alipaswa  kusherehekea kuzaliwa kwa binti yao ama kuomboleza kifo cha mwanawe.

"Sikuwahi kujua jinsi ya kuwa na furaha na huzuni kwa wakati moja. Ni vigumu kueleza. Hutaki kulia au kutabasamu kwa sababu ni jambo amblo linafanya usijue la kufanya,"

Ronaldo alifichua kuwa ameweka majivu ya Angél karibu na yale ya baba yake, ambaye alifariki  mwaka 2005 kutokana na matatizo ya ini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved