logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Shujaa 7s wanyakua shaba katika mashindano ya Edmonton 7s

Kenya ilichapa Canada 33-14 katika mechi ya mwisho na kumaliza katika nafasi ya tatu na pointi 16 nyuma ya Afrika Kusini na Uingereza ambao walichukua nafasi  ya kwanza na ya pili mtawalia

image
na Radio Jambo

Habari27 September 2021 - 02:48

Muhtasari


•Kenya ilichapa Canada 33-14 katika mechi ya mwisho na kumaliza katika nafasi ya tatu na pointi 16 nyuma ya Afrika Kusini na Uingereza ambao walichukua nafasi  ya kwanza na ya pili mtawalia

•Kwa sasa Kenya 7s imekalia nafasi ya tatu katika jedwali la World Rugby Series 2021 na jumla ya pointi 34 nyuma ya Afrika Kusini (40) na Uingereza (34).

Timu ya kitaifa ya raga, Kenya 7s almaarufu kama Shujaa 7s inaendelea kuandikisha msururu wa matokeo bora kwenye mashindano ya HSBC World Rugby Sevens Series ambayo yanaendelea.

Wiki moja tu baada ya Shujaa 7s kushinda medali ya fedha katika mashindano ya Vancouver 7s, vijana wa kocha Innocent Simiyu waliweza kujinyakulia nishani ya shaba kwenye mashindano ya Edmonton 7s ambayo yalichezwa nchini Canada wikendi ambayo imetamatika.

Kenya ilichapa Canada 33-14 katika mechi ya mwisho na kumaliza katika nafasi ya tatu na pointi 16 nyuma ya Afrika Kusini na Uingereza ambao walichukua nafasi  ya kwanza na ya pili mtawalia

Shujaa 7s walikosa nafasi .ya kuhitimu kuingia fainali baada ya kupoteza 7-33 dhidi ya miamba wa raga 'The Springboks' wa Afrika Kusini kwenye mechi ya nusu fainali.

Hapo awali Kenya ilikuwa imechapa Chile 38-5, Uhispania 26-12, Ujerumani 24-17 na kupoteza tena dhidi ya Afika Kusini 14-19.

Kwa sasa Kenya 7s imekalia nafasi ya tatu katika jedwali la World Rugby Series 2021 na jumla ya pointi 34 nyuma ya Afrika Kusini (40) na Uingereza (34).


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved