logo

NOW ON AIR

Listen in Live

ODM yaahirisha uchaguzi wa mchujo Nakuru

• Kupitia taarifa kwa wawaniaji wote Alhamisi usiku, Mumma alisema chama kilikuwa kimefutilia mbali kura za mchujo zilizopangwa kufanyika leo Aprili 1. 

image
na Radio Jambo

Habari01 April 2022 - 07:58

Muhtasari


• Kupitia taarifa kwa wawaniaji wote Alhamisi usiku, Mumma alisema chama kilikuwa kimefutilia mbali kura za mchujo zilizopangwa kufanyika leo Aprili 1. 

Catherine Mumma mwenyekiti wa bodi ya uchaguzi ya ODM

Mwenyekiti wa Bodi ya Kitaifa ya Uchaguzi ya ODM Catherine Mumma ameahirisha mchujo wa chama hicho mjini Nakuru kwa sababu alizosema ni za kiusalama. 

Kupitia taarifa kwa wawaniaji wote Alhamisi usiku, Mumma alisema chama kilikuwa kimefutilia mbali kura za mchujo zilizopangwa kufanyika leo Aprili 1. 

Bodi ya ychaguzi ilibaini kwamba hatua hiyo ilinuia kulinda maisha ya wanachama na viongozi na kwa hivyo iliwalazimu kusitisha kura za mchujo. 

Alitoa mfano ambapo maafisa Wasimamizi na makarani walipokea vitisho vya usalama kutoka kwa baadhi ya watu. Uamuzi wa uwakilishi wa wadi za Kaptembwa, Olkaria, Kivumbini na Shabaab utatolewa baadaye na kuwasilishwa kwa Wagombeaji. 

“Habari za jioni timu ya Nakuru!Hii ni kukufahamisha kuwa imetubidi kuahirisha uteuzi wa mchujo wa chama eneo la Nakuru na kuwasilisha uamuzi huu kwa kamati kuu,” taarifa bodi ya chaguzi ilisema. 

Mwenyekiti wa bodi ya uchaguzi aliomba radhi wawaniaji wote walioathiriwa na hatua hiyo lakini akasisitiza kwamba maisha yalikuwa muhimu sana.  

Hapo awali, wawaniaji na maafisa wa ODM katika kaunti walikuwa na kikao cha faragha na kuibua wasiwasi kuhusu waliochaguliwa kusimamia kura za mchujo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved