logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Pacha' wa rais Uhuru Kenyatta kuwania kiti cha Urais

Alisema amekuwa akitafakari suala la kuongoza taifa la Kenya kwa zaidi ya mwezi mmoja.

image
na Radio Jambo

Habari04 April 2022 - 02:32

Muhtasari


•Gitonga ambaye anatazamia kuwania kiti hicho cha juu zaidi kama mgombeaji huru alisema amekuwa akitafakari suala la kuongoza taifa la Kenya kwa zaidi ya mwezi mmoja.

•Aliwashambulia mafarasi wawili wakuu katika uchaguzi wa mwezi Agosti, Raila na Ruto huku akidai kwamba yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kuwakomboa Wakenya.

Jamaa kutoka mtaa wa Umoja  anayefanana na rais Uhuru Kenyatta kama shilingi kwa ya pili, Michael Njogo  Gitonga amejitosa rasmi kwenye siasa.

Gitonga ambaye alikuja kutambulika mwaka jana baada ya picha zake kuenezwa mitandaoni anaamini kuwa yeye ndiye bora kuridhi kiti kinachokaliwa na 'pacha' wake kwa sasa.

Akihutubia waandishi wa habari siku ya Ijumaa, Gitonga aliwashambulia mafarasi wawili wakuu katika uchaguzi wa mwezi Agosti, Raila na Ruto huku akidai kwamba yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kuwakomboa Wakenya.

"Sababu ya kuamua kuwa rais, nimeangalia nikaona Ruto na Raila hawawezi kusaidia watu. Wengine wanajiita hustler, mimi ni hustler halisi. Mimi ndiye nitakomboa  yule mwananchi wa chini. Najua mahitaji ya mwananchi wa chini na najua ile kazi inayomfaa," Alisema.

Gitonga ambaye anatazamia kuwania kiti hicho cha juu zaidi kama mgombeaji huru alisema amekuwa akitafakari suala la kuongoza taifa la Kenya kwa zaidi ya mwezi mmoja.

"Mimi sirudi nyuma. Huu si utani," Gitonga alisisitiza.

Gitonga atamenyana na wagombeaji wengine ambao tayari wametangaza azma yao wakiwemo Raila Odinga, William Ruto, Jimi Wanjigi, Reuben Kigame na wengineo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved