logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aladwa ataka ODM kumpa Wanyonyi tiketi ya ugavana Nairobi

“Bodi ya Uchaguzi impe Wanyonyi tikiti kama ilivyofanyika katika kaunti ya Kisumu na Mombasa".

image
na Radio Jambo

Yanayojiri19 April 2022 - 07:49

Muhtasari


• Wanyonyi ndiye mgombea wa pekee anayetaka kuteuliwa na chama cha ODM kwa kiti cha gavana wa Jiji la Nairobi lakini kufikia sasa hajapokea cheti cha uteuzi.

• Wanyonyi anatazamiwa kumenyana na Johnson Sakaja wa Kenya Kwanza.

 

Catherine Mumma mwenyekiti wa bodi ya uchaguzi ya ODM

Shinikizo zazidi kutolewa kwa chama cha ODM kupeana tikiti yake ya ugavana wa Nairobi moja kwa moja kwa mbunge wa Westlands Tim Wanyonyi.

Mbunge huyo wa Westlands ndiye mgombea wa pekee anayetaka kuteuliwa na chama hicho kwa kiti cha gavana wa Jiji la Nairobi lakini kufikia sasa hajapokea cheti cha uteuzi.

Hali hii sasa imemlazimu mbunge wa Makadara George Aladwa kujitosa kwenye mjadala huu na Kutaka chama hicho kitoe tikiti mara moja ili kumpa  Wanyonyi muda kuanza mikakati ya kushinda kiti cha ugavana katika uchaguzi wa Agosti.

“Ninaomba Bodi ya Kitaifa ya Uchaguzi ya ODM impe Tim Wanyonyi tikiti ya ugavana kama ilivyofanyika katika kaunti ya Kisumu, Migori, Homabay, Mombasa na Kakamega. Ndiye mgombeaji pekee na mwenye matumaini makubwa zaidi,” Aladwa alisema.

Aladwa alikuwa akizungumza siku ya Jumatatu, Aprili 18 alipoandamana na Wanyonyi kusambaza chakula cha msaada kwa familia 300 za Kiislamu kusherehekea Iftar.

Wanyonyi anatazamiwa kumenyana na Johnson Sakaja wa Kenya Kwanza ambaye tayari ametangazwa kuwa mgombeaji wa muungano wa Kenya Kwanza unaoongozwa na Naibu rais William Ruto.

Pia atachuana na mfanyabiashara Richard Ngatia (Jubilee) ambaye ameteua Philip Kaloki kama mgombe mwenza wake..

Chama tawala cha Jubilee kina wagombeaji, gavana wa sasa Anne Kananu, mfanyabiashara Agnes Kagure na Ngatia wanaotarajiwa kwenda kwa mchujo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved