logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Amason Kingi na chama chake cha PAA ahamia Kenya Kwanza

Kingi alisema waliafikiana kushughulikia matakwa ya Wapwani punde serikali ya Kenya Kwanza itakapoundwa.

image
na Radio Jambo

Makala10 May 2022 - 07:27

Muhtasari


• Baadhi ya sababu alizotaja ni kutofanikishwa kwa utaratibu wa kisheria kwa chama cha PAA kujiunga na muungano wa Azimio rasmi.

• Kingi pia alidai kwamba kuna usiri mkubwa katika oparesheni za muungano wa Azimio akisema kwamba hakuna uazi katika mikakati ya muungano huo.

Gavana wa Kilifi Amason Kingi

Chama cha Pamoja African Alliance (PAA) kimejiondoa kutoka muungano wa Azimio – One Kenya na kujiunga rasmi na muungano wa Kenya Kwanza.

Kinara wa chama cha PAA gavana wa Kilifi Amason Kingi akizungumza katika makaazi ya naibu rais mtaani Karen siku ya Jumanne alisema kwamba walilazimika kujiondoa kutoka muungano wa Azimio One Kenya kwa sababu mbali mbali.

Baadhi ya sababu alizotaja ni kutofanikishwa kwa utaratibu wa kisheria kwa chama cha PAA kujiunga na muungano wa Azimio rasmi.

Kingi pia alidai kwamba kuna usiri mkubwa katika oparesheni za muungano wa Azimio akisema kwamba hakuna uazi katika mikakati ya muungano huo.

Kulingana na sababu hizo Kingi alisema ilikuwa vigumu kwao kuendelea kushirikiana na muungano huo ili kuafikia agenda za chama hicho ambazo ni kupigania maslahi ya Wapwani.

Kingi pia alidai kwamba katika muungano wa Azimio – On Kenya hakuna agenda madhubuti inaoyolenga kuimarisha hali ya maisha ya watu wa pwani ili kuchochea maendelo katika kanda hiyo.

Gavana huyo wa Kilifi anayeondoka alisema kwamba baada ya mashauriano mafupi na ya kina na muungano wa Kenya Kwanza waliafikiana kushughulikia matakwa ya Wapwani punde tu serikali ya Kenya Kwanza itakapoundwa.

Miongoni mwa mambo mengine, Kingi alisema kwamba naibu rais William Ruto aliahidi kurejesha shughuli za baharini kutoka Naivasha hadi Pwani kama ilivyokuwa hapo awali.

Tangazo hilo la Kingi linajiri siku moja tu baada ya chama cha Maenedeleo Chap Chap kuhama muungano wa Azimio na kujiunga na Kenya Kwanza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved