logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mgombea urais ateketeza kadi ya wapiga kura baada ya kunyimwa kibali

Alikuwa mgombea wa mwisho kukataliwa ombi lake baada ya kukosa kufaulu mtihani wa IEBC.

image
na Radio Jambo

Uchaguzi06 June 2022 - 14:01

Muhtasari


  • Mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati alisema mgombeaji huyo aliwasilisha "rundo la nakala za vitambulisho kwa kaunti ambazo hazijabainishwa"

Mwaniaji urais Muthiora Kariara ameteketeza kadi yake ya mpiga kura baada ya kunyimwa kibali cha kugombea.

Kariara alijiwasilisha kwa IEBC katika ukumbi wa Bomas of Kenya ili kupata kibali siku ya Jumatatu wakati azma yake ilipogonga mwamba.

Alikuwa mgombea wa mwisho kukataliwa ombi lake baada ya kukosa kufaulu mtihani wa IEBC.

Mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati alisema mgombeaji huyo aliwasilisha "rundo la nakala za vitambulisho kwa kaunti ambazo hazijabainishwa".

Kati ya orodha ya wafuasi 20 ambayo aliwasilisha, Chebukati alisema, ni kaunti 19 pekee ndizo zilizopatikana kutii kanuni zilizowekwa.

Mgombea mwenza wake, aliongeza, hakuwa na kanuni za maadili zilizotiwa saini ambazo ni mojawapo ya stakabadhi za lazima ili kupata kibali. Wengine ni Gibson Ngaruiya, Dorothy Kemunto, James Kamau, Jeremiah Nyaga, Jane Juliet Munyeki, Peter Kingori, na George Munyotta. .

Mgombea wa Ford Asili Njeru Kathangu alikosa kufika mbele ya jopo la mchujo na kusababisha kuondolewa kwake.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved