logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Msiuze maisha yenu ya baadaye kwa machifu,'Gachagua awaonya vijana

"Kwa vijana wetu msikubali kuwauzia machifu Vitambulisho vyenu

image
na Radio Jambo

Habari06 August 2022 - 19:20

Muhtasari


  • Akizungumza katika uwanja wa Nyayo siku ya Jumamosi, alidai kuwa mipango ya kununua vitambulisho kutoka kwa vijana kutoka kwa machifu bado iko mbioni kuhakikisha kuwa hawapati kura

Mgombea mwenza wa DP Ruto Rigathi Gachagua amewataka vijana kutouza Kadi zao za Utambulisho kwa machifu kabla ya uchaguzi wa Jumanne.

Akizungumza katika uwanja wa Nyayo siku ya Jumamosi, alidai kuwa mipango ya kununua vitambulisho kutoka kwa vijana kutoka kwa machifu bado iko mbioni kuhakikisha kuwa hawapati kura.

"Kwa vijana wetu msikubali kuwauzia machifu Vitambulisho vyenu. Msiuze kesho yenu tunajua kuna mipango ya mkuu ya kununua vitambulisho," alisema.

Wakati huo huo, aliwaambia machifu wakae kwanza na wasiogopeshwe na maafisa wa Wizara aliodai kuwa wanawalazimisha kujihusisha kisiasa na uchaguzi.

“Tunataka kuwaambia machifu wanaodai kutishwa na wakubwa wa Wizara ya Mambo ya Ndani, msitishwe na wasijihusishe na siasa,” Gachagua aliongeza.

Mapema wiki hii, washirika wa Ruto wakilenga Wizara ya Mambo ya Ndani kwa madai ya kupanga kutumia machifu kuvuruga uchaguzi huo ili kumpendelea mgombea urais wa Azimio Raila Odinga.

Katika barua iliyomwandikia mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati ya Julai 30, UDA ilidai kuwa Ofisi ya Rais "inatuma maafisa wa polisi kutisha, kuwahangaisha na kuwashurutisha wapiga kura kumuunga mkono Raila."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved