logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wakabiliana na vijana huku ghasia zikishuhudiwa Kisumu

Machafuko yalizuka mwendo wa saa kumi na mbili unusu jioni baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 August 2022 - 21:33

Muhtasari


• Maafisa wa polisi wa kupambana na ghasia walilazimika kupiga vitoa machozi kuwatawanya vijana.

Ghasia zimezuka Kondele mjini Kisumu baada ya Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kumtangaza Naibu Rais William Ruto kuwa Rais mteule mnamo Agosti 15, 2022. Picha: DANIEL OGENDO

Ghasia zilizuka katika eneo la Kondele mjini Kisumu baada ya Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kumtangaza William Ruto kuwa Rais Mteule Jumatatu Agosti 15, 2022.

Machafuko ya ghafla yalizuka mwendo wa saa kumi na mbili unusu jioni baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais.

Wakazi hao walikabiliana na polisi katika mapigano ya paka na panya.

Picha: DANIEL OGENDO
Raia anaonekana kwenye baiskeli. Ghasia zimezuka Kondele mjini Kisumu baada ya Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kumtangaza Naibu Rais William Ruto kuwa Rais mteule mnamo Agosti 15, 2022. Picha: DANIEL OGENDO

Jumatatu kuanzia saa tisa alasiri, dalili za vurumai zilitanda katika mzunguko wa Kondele.

Maafisa wa polisi wa kupambana na ghasia walilazimika kupiga vitoa machozi, na kuwalazimu vijana waliokuwa wamejazana eneo hilo kukimbilia usalama wao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved