logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Mke wangu nikilala nje nikirudi anaangalia miguu kama ni safi ama chafu!

“Unajua mke wangu kitu cha kwanza nikifika kwa nyumba anaangalia miguu. Akipata niko msafi ananiuliza nimelala na nani. Akipata ni chafu anajua nimetoka kazini,” alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Vipindi04 April 2025 - 09:09

Muhtasari


  • Elias alifunguka zaidi kwamba mkewe amekuwa na hulka ya kumwangalia miguu kila anapolala kazini na kurudi alfajiri.
  • Kulingana na Elias, yeye hufanya kazi ya kusafirisha mchanga kwa lori na wakati mwingine hulala kazini kwa gari wanapochelewa, na pindi anaporudi alfajiri, kitu cha kwanza mkewe anafanya ni kumkagua miguu.

Ghost na Gidi

KATIKA kipindi cha Patanisho kwenye Gidi na Ghost Asubuhi ndani ya Radio Jambo, kijana kwa jina Elias mwenye umri wa miaka 23 kutoka Kisii aliomba kupatanishwa na mkewe Moraa mwenye umri wa miaka 20.

Elias alieleza kwamba mke wake alimkasirikia na kuenda kwao baada ya mama mkwe kupiga simu akitaka kuzungumza na mamake, jambo ambalo lilimfanya mkewe kuhisi kwamba alikuwa anasengenywa.

Kijana huyo alieleza kwamba hata hivyo, mkewe baada ya kufika kwao, mamake alimtaka kurudi katika ndoa yake ili kuyatatua na familia ya mumewe, na kweli akatii na kurudi japo bado alikuwa na hasira ndani ya nyumba.

Elias alieleza kwamba mkewe amekuwa na shida na mamake kiasi kwamba hawazungumzi na hata wakikutana njiani mmoja anaweza kanyaga mwenzake akipita.

“Tumekaa kwa ndoa kwa mwaka mmoja na tuko na mtoto mmoja, nilikosana na mke wangu wiki moja iliyopita baada ya mamake kupiga simu akitaka kuzungumza na mamangu,” Elias alieleza.

“Shida ilikuwa kwamba mke wangu hazungumzi na mamangu hata akipita njiani anaweza mkanyaga akienda, sasa mamangu akiniuliza mbona mke wako haniongeleshi na nikikaa na mke wangu kuzungumza naye nijue shida iko wapi nitatue, haniambii,” aliongeza huku akisisitiza mamake hajawahi mkosea mke wake.

Elias alisema mkewe alirudi kwa nyumba lakini hazungumzi naye na hata usiku wa jana hakulala kwa nyumba na baada ya kurudi asubuhi alimpata mkewe bado amemnunia na alitaka azungumziwe ili aache kununa.

Kwa bahati mbaya, Moraa alipopigiwa simu, alisikia sauti ya Elias na alipomtajia suala la mamake, Moraa alikata simu na kuzima.

Elias alifunguka zaidi kwamba mkewe amekuwa na hulka ya kumwangalia miguu kila anapolala kazini na kurudi alfajiri.

Kulingana na Elias, yeye hufanya kazi ya kusafirisha mchanga kwa lori na wakati mwingine hulala kazini kwa gari wanapochelewa, na pindi anaporudi alfajiri, kitu cha kwanza mkewe anafanya ni kumkagua miguu.

Mkewe akipata miguu ni safi, anamtuhumu kwamba alikuwa amelala kwa mwanamke aliyemuosha na akipata miguu ni chafu, anaridhika kwamba alilala kazini.

“Unajua mke wangu kitu cha kwanza nikifika kwa nyumba anaangalia miguu. Akipata niko msafi ananiuliza nimelala na nani. Akipata ni chafu anajua nimetoka kazini,” alisema.

“Akipata ni safi ananiambia rudi kwa huyo mwenye alikuwa amekuweka vizuri sasa kesi zinakuwa nyingi, sasa hiyo shinda ndio inakuwa kwa nyumba,” Elias aliongeza.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved