logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Nilimfumania mke wangu na mwanamume mwingine kitandani

Kulingana na bwana huyo hakuleta vurugu yoyote ilhali aliwaacha waendelee na kitendo chao.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri22 July 2021 - 05:39

Muhtasari


  • Nilimfumania mke wangu na mwanamume mwingine kitandani

Katika kitengo cha patanisho bwana Michael alituma ujumbe ili apatanishwe na mkewe ambaye alimvumania na mpango wake wa kando alipokuwa anatoka kazi.

Kulingana na bwana huyo hakuleta vurugu yoyote ilhali aliwaacha waendelee na kitendo chao.

"Naomba mnipatanishe na mke wangu wa miaka 10. Nilikuwa ninafanya kazi nje na kuja nyumbani baada ya miezi 2.

Siku moja nikarudi bila kumwambia nikampata na mwanaume mwingine kitandani... Sikuleta vurugu, nikamwambia wakimaliza waende mimi nikaondoka, akabeba vitu akaondoka

Aliniwachia watoto wawili baada yake kuondoka, ndio nilikuwa nalewa lakini niliacha nimeokoka sasa

Nilioa mke wa pili ambaye aliaga dunia baada ya kusumbuliwa na ujauzito," Alieleza.

Baada ya kufanya juhudi za kumfikia mke wake alikuwa na haya ya kusema;

"Huyu mwnamume alikuwa na mpango wa kando, ameuza shamb yote, pia alioa mwanamke mwingine na akaaga dunia huyo ni Mungu alikuwa amekataa, sitaki kurudiana naye,"

Kwa mengi zaidi tembelea radiojambo youtube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved