logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Jamaa amzuia mpenziwe kuenda shule, ataka waoane kwanza

"Nakupenda. Wewe ndo wangu wa maisha," Naomi alimwambi Samuel.

image
na Radio Jambo

Makala22 February 2023 - 05:26

Muhtasari


•Naomi alisema mchumba wake alikasirika baada ya kufahamu mipango yake ya kuendeleza masomo katika chuo kikuu.

•Samuel alisema kwamba hangeweza kuzungumza mengi kwa kuwa yupo kazini.

Ghost na Gidi

Brilliant Naomi ,21, kutoka Voi alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mchumba wake Samuel Mudema ambaye alikosana naye hivi majuzi.

Naomi alisema mchumba wake alikasirika baada ya kufahamu mipango yake ya kuendeleza masomo katika chuo kikuu.

Kaka yangu alikuwa anataka kunirudisha shule. Sikuwa nimemueleza. Nilimueleza baadae," alisimulia Naomi.

Aliongeza, "Alikuwa anataka niende  shule lakini alitaka niende baadae. Alitaka tuoane kwanza."

Samuel alipopigiwa simu, Naomi alichukua fursa hiyo kumuomba msamaha mpenzi wake kwa hatua aliyochukua.

"Sawa, nimekusamehe," Samuel alisema.

Samuel alisema kwamba hangeweza kuzungumza mengi kwa kuwa yupo kazini.

Hata hivyo, alimtaka mpenzi huyo wake kusimamisha mipango ya kuenda shule na kusubiri waingie kwenye ndoa kwanza.

"Avumilie kidogo. Tutaongea na yeye baadaye," alisema.

Naomi alimshukuru mpenzi huyo wake kwa kukubali msamaha wake.

"Nakupenda. Wewe ndo wangu wa maisha," alisema.

Gidi hata hivyo alimshauri mwanadada huyo kuangazia masomo yake kwanza kwa kuzingatia kuwa umri wake bado ni mdogo. Alimtaka kutofanya maamuzi kwa kuzingatia mapenzi ila maisha yake ya usoni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved