logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: "Hakunikosea, mapenzi ilipungua!" Mwanadada akiri kumblock mpenziwe bila sababu

Joan hata hivyo alikiri kwamba mapenzi yake kwa Eric yamepungua na akasema atamueleza sababu.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho07 March 2025 - 09:13

Muhtasari


  • Eric alisema mpenziwe alichukua hatua ya kumblock ghafla, bila sababu, baada ya kuchumbiana kwa takriban mwaka mmoja.
  • Joan alipopigiwa simu, aliweka wazi kwamba hana sababu haswa ya kumblock mpenziwe huyo wa mwaka mmoja.

Watangazaji wa Radio Jmabo

Kijana aliyejitambulisha kama Eric Ochieng (32) kutoka Kisumu alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na Joan Akinyi (27) ambaye alikuwa mpenzi wake.

Eric alisema mpenziwe alichukua hatua ya kumblock ghafla, bila sababu, baada ya kuchumbiana kwa takriban mwaka mmoja.

“Ata mimi sijui shida imetoka wapi. Tulikuwa tumechumbiana kwa kama mwaka mmoja. Tulishapanga tutaoana hivi karibuni. Mwezi uliopita aliamua tu kuniblock. Nikimpigia na number yoyote hashiki. Nilitaka nijue kama tunaweza kuelewana tuendelee na mahusiano,” Eric alisema.

“Mimi sikumkosea. Nashuku kuna mtu amekutana. Kuna wakati alikuja Kisumu mwaka jana Desemba na tulikaa naye siku mbili na hakuna kitu aliona kwa simu. Kurudi bado tulikuwa tunaongea. Hivi karibuni ameamua tu kuniblock. Hakuna mtu wa kwao nilijua,” aliongeza.

Joan alipopigiwa simu, aliweka wazi kwamba hana sababu haswa ya kumblock mpenziwe huyo wa mwaka mmoja.

“Hakuna kitu inaendelea. Nimemblock hivyo tu. Hakunikosea. Nilihitaji tu break. Hakuna mtu, niko serious,” alisema Joan.

Eric alimsukuma kumwambia ukweli ili ajue hatua ya kuchukua.

“Sijakublock, kama unataka kuongea na mimi nipigie moja kwa moja. Ukate simu unipigie tuongee,” Joan alimwambia.

Eric alisema, “Hana maneno mingi na ndio maana nampenda kama mke wangu.”

Joan hata hivyo alikiri kwamba mapenzi yake kwa Eric yamepungua na akasema kwamba kuna sababu.

“Kuna vile mapenzi imepungua. Kuna vitu mingi na siwezi sema, anipigie nimuelezee,” alisema.

Kwa upande wake, Eric alimwambia mpenziwe, “Bado nakupenda na vile tuliongea tukapanga ulikuwa uende nyumbani kwetu tuone. Unblock number yangu. Kama kuna mahali nilikosea naomba msamaha.”

Je, una ushauri ama maoni gani kuhusu Patanisho ya leo?

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved