logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Nilimhangaikia mke wangu kuenda Saudi, aliporudi hakuja kwangu na aliniacha na mtoto

“Nilikuachia mtoto ndio usinifuate eti nilienda na mtoto wako. Sitaki!” Naliaka alimwambia Ongura.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Patanisho14 March 2025 - 09:00

Muhtasari


  • Naliaka alieleza kwamba mumewe alimuonyesha madharau baada ya kumtumia pesa kisha akazima simu, na kusisitiza kwamba hii haikuwa mara ya kwanza bali ni mazoea ya Ongura.
  • “Huyo ni jamaa ambaye hasaidiki na hakusaidii pia,” Naliaka alisema.
  • Naliaka alimaliza kwa kumfichulia Ongura ukweli kwamba kwa sasa ameshaoleka kwingine na tayari ako na mimba.
Gidi na Ghost

ONGUSH Ongura, mwanamume kutoka kaunti ya Busia ni mwanamume mwenye msongo wa Mawazo baada ya kukosana na mkewe.

Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 32 alipeleka mahangaiko yake kwenye kitengo cha Patanisho kwa Gidi na Ghost kwenye Radio Jambo akiomba kupatanishwa na mkewe.

Kwa mujibu wa Ongura, walikosana na mkewe, Naliaka Simiyu mwenye umri wa miaka 28 baada ya kuenda Saudi Arabia na kurudi bila kurudi katika ndoa yake.

“Tumekuwa kwa ndoa kwa miaka tatu na tuko na Mtoto moja. Nilikosana na Bibi yangu mwaka wa 2022 baada ya mimi kukubali aende Saudi Arabia for 2yrs na alirudi May 2024. Baaya ya yeye kurudi hata hakufika nyumbani kwangu hata kwao pia. Akisikia sauti yangu kwenye simu anakata, mimi naomba nijue msimamo wake tu,” Ongura alieleza.

Alieleza kwamba walitoka nyumbani kuja Nairobi ambapo mkewe alipata nafasi ya kuenda Saudia na hadi ikaidi wakakubaliana kutoa mimba ambayo alikuwa nayo ilia pate kusafiri.

“Nilikuwa na mke nyumbani nikakuja Nairobi na yeye na tukaelewana akatoa mimba ili aende Saudi Arabia. Akafika huko baada ya mwaka akanitumia pesa 40k nikajenge nyumba. Nikamwambia siwezi jenga mpaka akuwe karibu akakasirika akaniblock. Hiyo pesa nikaongeza zingine nikanunua pikipiki. Sasa aliporudi hakufika kwangu na kwao hajaonekana,” Ongura alisema.

Alithibitisha kwamba mtoto ako na yeye na mkewe hajawahi fuatilia kuhusu maendeleo ya malezo ya mtoto wao.

Gidi na Ghost walipompigia Naliaka simu, alieleza kwamba hakuna cha kuelewana na mumewe.

Naliaka alieleza kwamba mumewe alimuonyesha madharau baada ya kumtumia pesa kisha akazima simu, na kusisitiza kwamba hii haikuwa mara ya kwanza bali ni mazoea ya Ongura.

“Huyo ni jamaa ambaye hasaidiki na hakusaidii pia,” Naliaka alisema.

Hata hivyo, mwanamume huyo alikubali makosa hayo na kusingizia ujana lakini akamuomba Naliaka kurudi kwa ajili ya kulea mtoto na kusema kwamba kwa sasa ameshakua kiakili.

Ni ombi ambalo Naliaka alikataa katakata kurudiana na yeye huku pia akidinda hata kutaka kumuona mwanawe.

“Nilikuachia mtoto ndio usinifuate eti nilienda na mtoto wako. Sitaki!” Naliaka alimwambia Ongura.

Naliaka alimaliza kwa kumfichulia Ongura ukweli kwamba kwa sasa ameshaoleka kwingine na tayari ako na mimba.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved