08 June 2021 1 Min Read
Mtu wa Ugali
Wakenya wamsherehekea 'Ugali man'
Charles Odongo amepongezwa na Wakenya wengi mitandaoni baada yake kupata kazi ya kufanya tangazo na kampuni ya kamari
In Summary
•Odongo alisisimua mitandao wiki mbili zilizopita baada ya video yake akila ugali na shauku kubwa alihusishwa kwenye tangazo lililochapishwa na kampuni ya Odibets siku ya Jumatatu.
Mkufunzi wa mazoezi kwa jina Charles Odongo amesherehekewa na Wakenya wengi mitandaoni baada yake kupata kazi ya kufanya tangazo na kampuni ya kamari ya Odibets.
Odongo ambaye alisisimua mitandao wiki mbili zilizopita baada ya video yake akila ugali na shauku kubwa alihusishwa kwenye tangazo lililochapishwa na kampuni ya Odibets siku ya Jumatatu.
The video could not be loaded.
Video from Charles Odongo
Wakenya wengi wameendelea kumpongeza Odongo ambaye kwa sasa ni mkufunzi wa mazoezi pande za Rongai huku wakimbatiza jina Ugali man.(mtu wa ugali)
Tazama hapa jumbe za Wakenya kwenye mtandao wa Twitter chini ya alama ya reli #UgaliMan
Tazama jumbe zingine za Wakenya wakimpongeza Odongo almaarufu kama Ugali Man chini ya alama ya reli #UgaliMan ( https://twitter.com/hashtag/UgaliMan?s=09 ) kwenye mtandao wa Twitter.