Nyota wa NBA, Tristan Thompson mwenye umri wa miaka 30 siku ya jumatatu alikiri ndiye Baba wa mtoto wa Maralee Nichols aliyezaliwa tarehe 1 Disemba.
Thompson ambaye ni baba wa watoto watatu kupitia ukurasa wake wa Instragram alieleza wazi kuwa yeye ni baba mtoto wa kiume aliyezaliwa hivi karibuni na mwanamke kutoka Huston baada ya kupata matokeo ya mtihani wa uzazi.
Isitoshe aliomba msamaha kwa mpenzi wa zamani na mama wa watoto wake, Khloe Kardashia
"Ninawajibika kikamilifu kwa matendo yangu. Kwa kuwa sasa ubaba umeanzishwa, natarajia kumlea mtoto wetu kwa amani. Ninaomba radhi kwa kila mtu niliyemuumiza au kumkatisha tamaa katika kipindi chote hicho" alinakiri