Aliyekuwa mpenzi wa Otile Brown, Nabayet almaarufu Nabii amejitokeza kwa mara ya kwanza na kuzungumza kwa mashabiki baada ya mahusiano yao ya miaka mitatu kufika hatima.
Kupitia ukurusa wake wa Instagram Nabii ameshukuru wote ambao wamekuwa wakimtumia jumbe wa kumjulia hali baada ya kutengana na mpenzi wake Otile Brown.
"Asante kwa kuchukua muda wenyu kunijulia hali na kunitumia ujumbe wa heri ya maisha. Upendo wenyu ni wa ajabu sana. Naendelea vizuri," alisema mpenzi wa Otile Brown Nabii
Siku ya Alhamisi Otile alitumia ukurusa wake wa instagramu kutangaza kuachana na Nabii.
Ikumbukwe wapenzi hao wamekuwa kwenye mahusiano kwa tabribani miaka mitatu, baada ya Otile kuachana na aliyekuwa mpenzi wake mwanasoshailiti Vera Sidika.