Mike Sonko amejitolea kusaidia mwanamke anayeshukiwa kuharibu mali ya mchumba wake.
Mwanamke huyo kwa jina Imelda Mwendwa Kiguda alikamatwa Jumatatu kwa madai ya kuharibu mali ya mpenzi wake baada ya kumfumania na mwanamke mwingine.
Mwanamke huyo anadaiwa kuharibu gari la mpenzi wake na kuvunja runinga yake alipompata mpenzi wake akiwa kwenye tendo hilo.
Alipofikishwa kortini binti huyo alitakiwa kulipa dhamana ya pesa taslimu sh100,000.
Mike Sonko alichapisha kwenye akaunti yake ya Twitter kuashiria kutorithika na umauzi huo wa mahakama kuhusu suala hilo.