In Summary
  • Mashabiki wamuonya Flaqo baada ya kumkejeli rappa Octopizzo
flaqo-324x235

Erastus Ayieko Otieno maarufu  Flaqo ni mmoja wa wasanii na wachekeshaji wengi wanaosherehekewa  nchini Kenya.

Yeye ni ufafanuzi wa kweli wa kutia bidii katika kazi yake tangu alipoanza kazi ya ucheshi  akawa na mafanikio zaidi kuliko watu waliokuwa katika sekta ya burudani mbele yake. 

Maudhui yake kwa kawaida yanategemea masuala yanayohusiana na jamii ikiwa ni pamoja na nyumba za Afrika, shule kati ya mengine.

Flaqo alipakia  video yake mwenyewe akiiga jinsi Octopizo huwa anaandika nyimbo zake.

Alitumia sauti ya  Octopizzo lakini alitumia maneno ya kupendeza ili kuunda mistari.

Baadhi ya mashabiki wake walifuahishwa na video hiyo, huku wengine wakimuonya kuwa atapokea kichapo, kwa ajili ya kitendo hicho alimfanyia Octopizo.

Hizi hapa jumbe za mashabiki;

tosh_muriithi: 😂kijana utamadwa😂

bencyco: What's wrong with you man?😂😂😂

bandanafather: 😂😂utapigwa😂😂😂😂

elkavio_jnr: Umeamua V for violens😂😂😂

its_vijay_vick_the_dj: 😂😂😂😂saizi ako anaandika Noma niko maganji 🔥🔥🔥🔥

mr_kakerea_: Pizoo dee😂😂 Kin'g en yu know et!😂

being_ayalaa: Utagongwa msee

 

 

View Comments