Msanii Iyanii aliwashangaza mashabiki baada ya kuwasili katika hafla ya uzinduzi wa album ya Arrow Bwoy akiwa uchi.
Akizungumza kwenye mahojiano na mwanablogu Mungai Eve, Iyanii alisema kwamba vazi hilo [chupi na karatasi ya nailoni] lilimgharimu zaidi ya shilingi laki moja.
Iyanii alisema alichagua vazi hilo kwa kuwa yeye ni msanii ambaye analenga matao ya kimataifa kwa hivyo lazima hatua yoyote anayopiga iwe na ukali wa aina yake.
Aliongeza kwamba alinunua vazi hilo kutoka taifa ya Ufaransa.
Aidha mwanamuziki huyo alisema kwamba hakufanya hivo ili kujenga mazingira ya kusukuma album ya Arrow Bwoy, na kujitetea kuwa amekuwa akitoa ngoma kali ambazo zimependwa na mashabiki wengi.