In Summary

 

  •  Rais Trump na mkewe ni miongoni mwa walioambukizwa corona lakini sasa wamepona 
  • Maafisa wengine wa White House pia walipatwa na maradhi hayo 

 

Melania Trump

Mtoto wa kiume wa rais wa Marekani  Donald Trump  Barron ,mwenye umri wa miaka 14 aliambukziwa virusi vya corona  lakini sasa amepona ,amesema mke wa rais Melania Trump

 Melania alisema hofu yake iligeuka kuwa ukweli wakati  Barron alipopatiukana na virusi hivyo  lakini amesema kwa bahati  nzuri ‘ni kijana mwenye nguvu ‘ na hakuonyesha daalili zozote .

 Rais Trump na Melania  walipatikana na virusi hivyo  pamoja na wafanyikazi wengine wa White House  lakini wamepona . Trump pia alithibitisha kwamba mwanawe alikuwa na corona kwa kusema  kwamba ‘ alikuwa na ugonjwa huo kwa muda mfupi’ wakati wa mkutano wa kampeini  katika jimbo la Iowa .

 Kura za maono zaonyesha kwamba Trump yupo nyuma ya mpinzani wake  Joe Biden  huku zikisalia wiki tatu tu kabla ya uchaguyzi wa Novemba tarehe 3  lakini ushindani kato yao umejibana sana katika majimbo mengi muhimu

 Bwana Boden hakuwa na mikutano ya kampeini siku ya jumatano lakii alifanya hafla ya mchango kupitia njia ya mtandao na kutuma ujumbe uliorekodiwa kwa shirika la waislamu nchini marekani .   Mrengo wa Biden ulitangaza kwamba ulipata mchango wa  dola milioni 294 mwezi septemba .

 

View Comments