Mchekeshaji wa Churchill show Ben Morris anayefahamika kwa jina lake la usanii Othuol Othuol ameaga dunia .
Staa huyo wa jukwaa la vituko aliaga dunia katika hospitali ya KNH ambako amekuwa akipokea matibabu baada ya kupatikana na uvimbe katika ubongo wake
Mwanzilishi wa kipindi hicho Danile Ndambuki amethibitisha kifo cha Othuol akiandika katika mitandao ya kijamii ;
‘Maisha ni mafupi .Mungu hutoa na mungu huchukua .Sote tuko safari . Lala salama Othuol’
Othuol amekuwa nje na ndani ya hospitali kwa muda .Wiki chache zilizopita alikimbizwa hospitalini huku marafiki na jamaa zake wakiwataka wakenya kumuombea . Wakenya wengi wamefurika mitandao ya kijamii kumuomboleza Othuol .