Mahakama ya Nairobi imetupilia mbali kesi dhidi ya mwalimu aliyehusishwa na kifo cha seneta wa machakos Boniface Kabaka ambaye alikuwa amezuiliwa na kisha kuachiliwa huru baadaye kwa sababu ya ukosefu wa ushahidi .
Mahakama siku ya alhamisi ilifutilia mbali kesi iliyokuwa ikimkabili Bi Esther Muli . Hii ni baada ya DPP kuwasilisha ombi la kuiondoa kesi hiyo akisema ushahidi ulitolewa haukumuweka mtuhumiwa katika eneo la kifo cha marehemu Kabaka .
Upande wa mashtaka umesema uchunguzi wa watalaam umebaini kwamba hakuna ushahidi unaomhusisha mshukiwa na kifo cha kabaka
Hakimu mkuu David Ndungi akimuachilia Muli amesema amezingatia ombi lililotolewa na Mkurugenzi wa mashtaka ya umma .