logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Laghaiwa kwa gharama ya akili yako ndogo" Zari awaambia wanaokubali kulaghaiwa

Mwanasosholaiti Zari Hassan amesema kuwa yeye huwa haombi msaada wa fedha wala kupeleka watu ughaibuni

image
na Radio Jambo

Makala20 May 2021 - 12:20

Muhtasari


•Zari amesema kuwa yeye huwa haombi msaada wa fedha wala kupeleka watu ughaibuni

•Asema huwa hatumi jumbe za Facebook na Instagram wala kujibu jumbe anazotumiwa

Zari Hassan

Mwanasosholaiti na mwanabiashara maarufu Zari Hassan amewaonya watu wanaolaghaiwa mitandaoni na wakora wanaojitambulisha kama yeye.

Zari ambaye alikuwa mpenzi wake Diamond Platnumz amesema kuwa hatokubali kamwe kukubali wajibu kwa tendo asilohusika.

“Huwa siombi msaada wowote wa kifedha na siwapeleki watu ughaibuni. Siagizi pesa zozote kufanya  Zari, sifanyi hilo” Zari aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Binti huyo mzaliwa wa Uganda ameonekana kukasirishwa na kitendo cha mmoja wa wakora wanaomuiga kulaghai watu na kisha waliolaghaiwa kumtumia Zari barua pepe wakidai kurudishiwa fedha zao.

Wanaonijua wanaelewa kuwa huwa situmi jumbe za Facebook na huwa sijibu jumbe ninazopokea kwenye mtandao huo.” Zari alisema huku akimueleza aliyelaghaiwa aonyeshe nambari ya WhatsApp aliyokuwa anazungumza nayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved