logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Staa wa dancehall kutoka Jamaica Sean Paul athibitisha atatumbuiza nchini Kenya, atoa maelezo

Tikiti za tamasha hilo zinauzwa kuanzia Sh3000 hadi 120,000.

image
na Samuel Mainajournalist

Burudani29 October 2024 - 10:02

Muhtasari


  • Msanii huyo wa dancehall mwenye umri wa miaka 51 alithibitisha kwamba atatumbuiza katika jiji la Nairobi mnamo mwezi Desemba.
  • Staa huyo wa dancehall atatumbuiza katika jiji kuu la Kenya mnamo Desemba 1, 2024.

Mwimbaji mkongwe wa Jamaica Sean Paul Ryan Francis Henriques OD almaarufu Sean Paul atafanya ziara ya Kenya mwishoni mwa mwaka huu wa 2024.

Mnamo siku ya Jumatatu, Oktoba 28, msanii huyo wa dancehall mwenye umri wa miaka 51 alithibitisha kwamba atatumbuiza katika jiji la Nairobi mnamo mwezi Desemba.

Sean Paul aliwataka mashabiki wake kuandaa tiketi zao huku wakisubiri kumtazama akitumbuiza moja kwa moja jukwaani.

“Nani kasema siji jijini Nairobi? Pata tiketi yako sasa!” Sean Paul alisema Jumatatu jioni kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Mwimbaji huyo aliambatanisha chapisho lake na kiungo ambapo mashabiki wanaweza kupakua tikiti zao kutoka.

Kulingana na bango la shoo hiyo lililosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, staa huyo wa dancehall atatumbuiza katika jiji kuu la Kenya mnamo Desemba 1, 2024.

Sean Paul atatumbuiza pamoja na baadhi ya wasanii wa Kenya wakiwemo Redsan, G-Money, CNG, Dream, Sir Effexy, Mish, ZJ Heno, Motif Di Don na kundi la wasanii wa arbantone.

Tikiti za tamasha hilo zinauzwa kuanzia Sh3000 kwa shabiki wa mapema hadi 120,000 kwa kundi la kitengo cha dhahabu la watu 6.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved