logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Kuolewa Ni Constant!” Akothee Adokeza Harusi Nyingine Ya 3 Itakayokuwa Funga-Kazi

Hata hivyo, alionesha Imani ya ndoa yake ya mwisho na Nelly Oaks kuwa na mafanikio akisema kuwa isipofanya kazi bado atarudi sokoni kujaribu harusi kwa mara ya 4.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani09 December 2024 - 10:31

Muhtasari


  • Hata hivyo, alionesha Imani ya ndoa yake ya mwisho na Nelly Oaks kuwa na mafanikio akisema kuwa isipofanya kazi bado atarudi sokoni kujaribu harusi kwa mara ya 4.
  • Itakumbukwa mwaka jana, Akothee alisimamisha jiji la Nairobi na mitandao ya kijamii mnamo Aprili alipoamua kufunga harusi ya kifahari.



MSANII na mjasiriamali Esther Akoth Kokeyo, maarufu kama Akothee amedokeza kwamba bado hajafa moyo katika kusimika penzi lake kwenye ndoa ya harusi.


Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Akothee alichapisha picha zake za zamani na kuweka wazi kwamba kama kuna jambo hawezi kuchoka kulifanya, basi ni kufunga harusi.


Alisema kwamba hivi karibuni, atafunga harusi nyingine ya 3 ambayo aliitaja kuwa itakuwa ya mwisho kabisa katika maisha yake ya kusaka mapenzi.


Mama huyo wa watoto 5 alidokeza kuwa ndoa hiyo ya tatu itakuwa baina yake na mpenzi wake wa muda mrefu, Nelly Oaks ambaye alimtaja kama ‘partner in crime’.


“KUOLEWA KWA AKOTHEE NI CONSTANT. Harusi yangu ijayo ya 3 na pengine ya mwisho itakuwa nzuri zaidi kwa sababu nitakuwa nikioana na mpenzi wangu katika uhalifu,” Akothee alisema.


Akionekana kutupa dongo kwa penzi lililosambaratika na wapenzi wa awali, alisema kuwa wapenzi wake – akiwemo Denis Schweizer maarufu kama Mr Omosh, walikuwa ni walanguzi wa mapenzi tu.


Hata hivyo, alionesha Imani ya ndoa yake ya mwisho na Nelly Oaks kuwa na mafanikio akisema kuwa isipofanya kazi bado atarudi sokoni kujaribu harusi kwa mara ya 4.


Aliwataka mashabiki wake kutolalamika kuhusu idadi ya harusi atakazofanya, akiwaambia kwamba lao litakuwa tu kununua vitenge na kwa wale watakaokuwa mbali yao itakuwa kununua bundles ili kufuatilia mtandaoni.


“Hawa wengine walikuwa Criminal wa mapenzi. Sasa hii ni kweli halisi. Na hii ya tatu isopofanya vizuri, Tutakuwa na another last one wewe kazi yako iwe ni kushona kitenge na bundles,” Akothee alisema.


Itakumbukwa mwaka jana, Akothee alisimamisha jiji la Nairobi na mitandao ya kijamii mnamo Aprili alipoamua kufunga harusi ya kifahari.


Harusi hiyo iliandaliwa kwa mtindo wa kifahari ambapo alisema ‘NDIO’ kwa mpenzi wake wakati huo, raia kutoka Uswizi, Denis Schweizer aliyekuwa amempa jina Mr Omosh na hata kumfungulia akaunti za mitandao ya kijamii kwa jina hilo.


Hata hivyo, miezi 5 baadae, ndoa hiyo ilisambaratika na ilimchukua Akothee muda mrefu kukubali ukweli huo na hata kuusema wazi kwa mashabiki wake mtandaoni.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved