logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akothee Kutoa Msaada Wa Kimasomo Kwa Mayatima Walio’trend Kwenye Jeneza La Mzazi

“Nitatoa chakula, elimu, malazi, matibabu, na usaidizi mwingine wowote wa kimama wanaohitaji,” Akothee aliahidi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani07 January 2025 - 08:01

Muhtasari


  • Mmoja wa watu ambao wameomba kusaidiwa kufikia watoto hao ni Akothee ambaye ameahidi kuwapa msaada wa kimasomo watoto hao katika shule yake ya Akothee Foundation.



MSANII NA MJASIRIAMALI Esther Akoth Kokeyo maarufu kama Akotee ameahidi kutoa msaada wa kimasomo kwa watoto 4 mayatima ambao picha yao ya kutia huruma wakiwa kwenye jeneza la marehemu mzazi wao ilevutia hisia nyingi na nzito mitandaoni.


Watoto hao wadogo 4 walisimamishwa mbele ya jeneza la mzazi wao kwa picha ya mwisho ya kumbukumbu, na picha hiyo imevutia hisia nyingi na nzito miongoni mwa watumizi wa mitandao.


Hata hivyo, haijulikani hafla hiyo ya mazishi hayo ya kutia huruma ilifanyika wapi, lakini watu wengi wameomba msaada wa jinsi wanaweza fikia familia hiyo changa iliyoachwa.


Mmoja wa watu ambao wameomba kusaidiwa kufikia watoto hao ni Akothee ambaye ameahidi kuwapa msaada wa kimasomo watoto hao katika shule yake ya Akothee Foundation.


Msanii huyo aliomba mtu yeyote anayeweza kumpa msaada wa kuwafikia kujitokeza, akisema kuwa japo shule yake si ya bweni, lakini angeomba kuwasaidia mradi tu wawe na mtu angalau mmoja kutoka kwa uko atakayewatunza ili kufikia masomo kwa kutwa.


“Moyo wangu umeumizwa na kuona watoto hawa. Je, kuna yeyote aliye na habari kamili au maelezo kuhusu jinsi tunavyoweza kusaidia? Ingawa shule yangu bado si taasisi ya bweni, ikiwa wana mlezi au mwanafamilia aliyesalia, niko tayari kuwahifadhi chini ya uangalizi na mwongozo wa ndugu zao wa damu.”


“Nitatoa chakula, elimu, malazi, matibabu, na usaidizi mwingine wowote wa kimama wanaohitaji,” Akothee aliahidi.


“Walakini, ni muhimu kwamba waambatane na mtu wa familia. Ulimwengu unaweza kuwa wa kikatili sana, lakini kwa pamoja, tunaweza kuleta mabadiliko. Mungu akubariki mwaka huu kwa kugusa mioyo,” aliongeza mama huyo wa watoto 5.


 


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved