logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbosso Yuko Mbioni Kuondoka WCB Na Diamond Amemruhusu Bila Malipo!

Baba Levo alifichua kwamba Diamond amemruhusu Mbosso kuondoka bila kulipia gharama ndefu kama watangulizi wake – Rayvanny, Harmonize na Rich Mavoko.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani30 January 2025 - 10:38

Muhtasari


  • Levo alisema kwamba Mbosso ametamkiwa Baraka zote na bosi wake kuondoka ili kuendelea kuipambania nyota yake kimuziki nje ya WCB Wasafi. 
  • Watangulizi wake katika kuondoka WCB ni pamoja na Harmonize, Queen Darleen, Rayvanny na Rich Mavoko.
  • Kuondoka kwake kutamaanisha kwamba Diamond atasalia na wasanii watatu tu – Zuchu, Lavalava na D Voice ambaye alisajiliwa na WCB Novemba 2023.



MSANII Mbosso Khan yuko mbioni kuondoka katika lebo ambayo imemkuza ya WCB Wasafi muda wowote kutoka leo hii.


Haya ni kwa mujibu wa rafiki na chawa wa karibu wa bosi wa lebo hiyo, Baba Levo ambaye amefichua kwamba Diamond Platnumz tayari ameshalipitisha suala la msanii huyo kuondoka.


Baba Levo alifichua kwamba Diamond amemruhusu Mbosso kuondoka bila kulipia gharama ndefu kama watangulizi wake – Rayvanny, Harmonize na Rich Mavoko.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo kutoka kwa Baba Levo, Diamond amemsamehe Mbosso gharama hizo zote na kumruhusu kuondoka bila kulipia hata senti kutokana na nidhamu kubwa ambayo ameionyesha tangu ajiunge na WCB.


Levo alisema kwamba Mbosso ametamkiwa Baraka zote na bosi wake kuondoka ili kuendelea kuipambania nyota yake kimuziki nje ya WCB Wasafi.


“Kutokana na heshima kubwa ya Mbosso kwa Diamond na viongozi wa WCB, Lukuga [Diamond] amemfungulia milango Mbosso akajitafutie mwenyewe bila kulipa chochote WCB.”


“Nidhamu Kubwa Ya MBOSSO Imemfanya @diamondplatnumz Amsemehe MAMILIONI YA PESA Na Kumpa UHURU WA KWENDA KUPAMBANA NNJE YA WCB,” Baba Levo aliakisi.


Aidha, chawa huyo wa Diamond alizidi kutoa taarifa zaidi akifichua kwamba Diamond na uongozi wake baada ya kuondoka kwa Mbosso watasaini wasanii wapya 9.


“Hii Inawapa NAFASI WCB KUSAINI WASANII WENGINE WAPYA MWAKA HUU 2025,” Baba Levo alifichua.


https://www.instagram.com/p/DFat_yiNP4L/

Mbosso, ambaye jina lake halisi ni Mbwana Yusuph Kilungi alianza kazi yake ya muziki mnamo 2013 kama mwanachama wa Yamoto Band, ambapo alienda kwa jina la kisanii "Maromboso".


Mnamo 2018, alisaini na WCB Wasafi, lebo ya rekodi iliyoanzishwa na Diamond Platnumz.


Mbosso ametoa vibao vingi vilivyoongoza chati, vikiwemo "Maajabu", "Picha Yake", "Tamu", "Tamba" miongoni mwa mashairi mengine mengi na kumfanya kujinafasi miongoni mwa mastaa tajika wa muziki Afrika Mashariki.


Ikiwa ni kweli ataondoka, basi atakuwa msanii wan ne kugura lebo hiyo inayoaminika kuwa bora zaidi Afrika Mashariki.


Watangulizi wake katika kuondoka WCB ni pamoja na Harmonize, Queen Darleen, Rayvanny na Rich Mavoko.


Kuondoka kwake kutamaanisha kwamba Diamond atasalia na wasanii watatu tu – Zuchu, Lavalava na D Voice ambaye alisajiliwa na WCB Novemba 2023.


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved