logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Msanii hakutengeneza pesa wakati wa bifu yangu na Pozee atakufa maskini!” – Bahati

Wawili hao wameachia kolabo mbili kwa mpigo, Paah na Keki ambazo zimeshuka asubuhi ya Ijumaa kwenye majukwaa ya kidijitali ya kupakua miziki.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani31 January 2025 - 10:57

Muhtasari


  • Alhamisi, wawili hao ambao wamekuwa wakihasimiana kwa miaka kadhaa walitangaza kuja Pamoja na kuachia kolabo mbili kwa mpigo.
  • "Hivyo kama kuna msanii hakutengeneza pesa huo wakati ajue sasa atakufa maskini maana sisi tumerudi,” Bahati alisema. 



MSANII wa EMB Records, Bahati Kioko ametoa tamko la kejeli kwa wasanii wengine akisema kwamba kama walishindwa kutengeneza pesa wakati yeye na Willy Paul walikuwa hawapatani basi asahau kuwa Tajiri.


Bahati alikuwa anazungumza katika video moja akiwa na Willy Paul katika maandalizi ya mwisho kuelekea kuachiliwa kwa kolabo yao.


Bahati alidai kwamba kama kuna msanii yeyote aliyeshindwa kuchukua fursa ya bifu lake na Willy Paul kutengeneza pes abasi atakufa maskini kwani wawili hao tayari wamerekeisha urafiki wao.


Alijipiga kifua akisema kwamba yeye na Willy Paul ndio wasanii pekee wamekuwa wakishikilia tasnia ya burudani nchini kwa miaka 10, na kama hiyo haitoshi, ndio tena wameanza upya wakiwa marafiki.


“Unajua sasa hivi ndio tumeanza, ni enzi mpya na ujue bado sisi ndio tumekuwa tukishikilia kwa miaka 10 na ndio tunaanza tena. Hivyo kama kuna msanii hakutengeneza pesa huo wakati ajue sasa atakufa maskini maana sisi tumerudi,” Bahati alisema huku Willy Paul akimuunga mkono kwamba hii ni enzi ya kuwafuuza wasanii wa kigeni kutoka kilele cha chati za muziki humu nchini.


Alhamisi, wawili hao ambao wamekuwa wakihasimiana kwa miaka kadhaa walitangaza kuja Pamoja na kuachia kolabo mbili kwa mpigo.


Walitangaza kolabo hizo zingeshuka mapema Ijumaa asubuhi na upekuzi wa haraka, tayari kufikia muda wa kuchapishwa kwa ripoti hii walikuwa wameachia ngoma ya kwanza kwa jina ‘Paah’.


Ngoma nyingine ambayo wamefanya Pamoja na ambayo ingeshuka muda sawia inaitwa ‘Keki’.


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved