logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Simple Boy Apiga Magoti Na Kusujudu Baada Ya Kuzawadiwa Gari, Mazda Demio

Alionyesha picha kadhaa akiwa amepiga magoti na kusujudu kando na gari hilo lenye rangi ya divai

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 February 2025 - 12:42

Muhtasari


  • Alionyesha picha kadhaa akiwa amepiga magoti na kusujudu kando na gari hilo lenye rangi ya divai.
  • “Asante @khushimotorskenya kwa zawadi, asante boss @wakasgondal kwa neema, MUNGU akubariki,” Stevo alichapisha.

Stevo Simple Boy afurahi kutunukiwa gari jipya aina ya Mazda Demio

RAPA Stevo Simple Boy ni msanii mwenye furaha baada ya kampuni moja ya kuuza magari humu nchini kumpa zawadi ya gari jipya.

Msanii huyo ambaye alianza maisha ya kuhangaika katika mitaa ya mabanda ya Kibera sasa ni mmiliki mpya wa gari aina ya Mazda Demio katika jiji la Nairobi.

Stevo Simple Boy alivunja taarifa hizi kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo alionyesha picha kadhaa akiwa amepiga magoti na kusujudu kando na gari hilo lenye rangi ya divai.

Katika picha nyingine, Stevo Simple Boy alionekana akiwa amelilalia gari hilo kama anayetaka kulikumbatia kwa furaha na kushukuru kampuni hiyo na mmiliki wake kwa neema hiyo ya ajabu.

“Asante @khushimotorskenya kwa zawadi, asante boss @wakasgondal kwa neema, MUNGU akubariki,” Stevo alichapisha.

Msanii huyo ambaye katika sehemu kubwa ya mwishoni mwa mwaka jana na mapema mwaka huu amekuwa akifanya vizuri katika vitimbi vyake mitandaoni amejizolea umaarufu usio na kifani.

Mwishoni mwa mwaka jana, Stevo alikamilisha ziara yake kwenda nchini Tanzania, katika kile ambacho alikitaja kuwa alikuwa katika mishe za kufuatilia kolabo yake na bosi wa lebo ya Konde Gang, Harmonize.

Hata hivyo, licha ya kutofanikiwa kukutana naye, Stevo alisema kwamba mwaka huu hilo litakuwa moja ya ajenda zake kuu kuhakikisha wanafanikisha kolabo na mkali huyo wa zamani kutoka lebo ya WCB Wasafi.

Bila shaka kupata gari ni hatua kubwa kwa juhudi zake kimuziki na wengi wanahisi meneja wake mpya, Machabe amekuwa moja kati ya mihimili ya kumfanikishia Simple Boy ndoto zake, haswa baada ya wengi kudhani nyota yake ingedidimia baada ya kufeli mikononi mwa mameneji wawili wa awali.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved