logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bradley Mtall amtongoza mtangazaji wa NTV Live kwenye kipindi, adai yeye sasa Muislamu!

"Lakini hata kama Amina uko na mtu, unajua hata kugongewa ni constant,” Bradley alimshinikiza zaidi Amina kukubali ombi lake.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani05 April 2025 - 09:15

Muhtasari


  • Bradley alifunguka kwa Amina kwamba amekuwa akimtolea jicho la kumtamani na mara kwa mara hata kabla wakutane kwenye studio za NTV, alikuwa akimsumbua meneja wake – Director Trevor – kumtafutia jinsi ya kuwasiliana na Amina.
  • Bila kupiga kona na kuenda njia ndefu, Bradley alimkabili Amina moja kwa moja na swali la kutaka kujua kama ana mume au la, akiwa na lengo la kutaka kujaza hilo pengo kama jibu lake lingekuwa la!

Bradley Mtall amrushia mistari mtangazaji Amina Rabar wakiwa kwenye studio za NTV//FACEBOOK

KIJANA mrefu zaidi humu nchini Bradley Marongo maarufu kama Gen Z Goliath ama Bradley Mtall amefunguka kwamba yeye kwa sasa ni Muislamu baada ya kile alichodai kwamba amebadili dini hivi majuzi – hivyo anaweza oa wanawake hadi 4.

Akizungumza moja kwa moja kwenye runinga ya NTV, Bradley Marongo, alionyesha uhodari wake baada ya kujaribu kurusha mistari yake kwa mtangazaji wa kipindi Amina Abdi Rabar.

Bradley alifunguka kwa Amina kwamba amekuwa akimtolea jicho la kumtamani na mara kwa mara hata kabla wakutane kwenye studio za NTV, alikuwa akimsumbua meneja wake – Director Trevor – kumtafutia jinsi ya kuwasiliana na Amina.

Bila kupiga kona na kuenda njia ndefu, Bradley alimkabili Amina moja kwa moja na swali la kutaka kujua kama ana mume au la, akiwa na lengo la kutaka kujaza hilo pengo kama jibu lake lingekuwa la!

“Unajua huwa nasumbua Trevor kila siku nikimwambia Trevor nitafutie namba ya Amina. Namwambia Trevor mimi nataka Amina, nimemcrushia Amina. Trevor aliniambia Hapana Amina ako na bwana, sasa ndio nataka uniamie leo uko na bwana ama Hapana?” Bradley Marongo alimuuliza Amina bila kupepesa jicho.

Hata hivyo, Amina alimvunja moyo kwa kumwambia kwamba yeye ni mke wa mtu lakini Bradley hakukaa kinyonge, alijitetea kwamba yeye sasa hivi ni muislamu na ana uwezo wa kuishi katika ndoa ya mitala.

“Sasa unajua mimi ni Muislamu na tunaruhusiwa kuoa bibi watatu hadi wanne. Jina langu la Kiislamu kwa sasa ni Ishmael. Lakini hata kama Amina uko na mtu, unajua hata kugongewa ni constant,” Bradley alimshinikiza zaidi Amina kukubali ombi lake.

Kijana huyo anayejidai kuwa na urefu wa zaidi ya futi 8 alijizolea umaarufu mwaka jana, shukrani kwa harakati za maandamano ya vijana wa Gen Z ambapo alionekana na kuvutia umakini wa wengi.

Tangu wakati huo, Bradley amekuwa kipenzi cha wengi kiasi kwamba kila anayekutana naye anaingiwa na uchu wa kutaka kupiga picha naye.

Amekuwa akisimamiwa na Director Trevor ambaye kupitia kwake Bradley amepata dili kibao za kuwa balozi wa mauzo ya kampuni za bidhaa mbalimbali ndani na nje ya Kenya.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved