logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hata kama Jay-Z ni bilionea, utajiri wake haushindi utajiri wa ng’ombe wangu – Muhoozi

“Eti Jay-Z ni bilionea? Huo ni utani! Ng'ombe wangu wana thamani kuliko yeye!” Muhoozi alihoji huku akidai kuwa atampokonya Jay-Z mke wake Beyonce na kumhamishia Uganda.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani06 April 2025 - 09:55

Muhtasari


  • Lakini je, ni kweli kwamba utajiri wa ng’ombe wa mwanawe Museveni unazidi maradufu utajiri wa msanii Jay-Z kutoka Marekani?
  • Kwa mujibu wa ripoti ya Forbes ya mwaka 2024, Jay-Z ndiye msanii Tajiri zaidi duniani akiongoza kwa utajiri wa dola bilioni 2.5 – sawa na shilingi bilioni 323 za Kenya.
Muhoozi amtania Jay-Z kuhusu utajiri wa ngombe wake

JENERALI mkuu wa majeshi ya Uganda UPDF, Muhoozi Kainerugaba ameanzisha tena upya vita vyake vya mtandaoni dhidi ya msanii mkwasi kutoka Marekani, Jay-Z.

Mwanawe rais Yoweri Museveni sasa ameibuka na madai mapya kwamba msanii huyo bilionea hakustahili kuwa na mwanamke kama Beyonce, akisisitiza kwamba mrembo huyo ni wake.

Kupitia ukurasa wake wa X, Muhoozi Kainerugaba amedai kwamba hata kama Jay-Z ni bilionea – hadhi aliyoitaja kwamba kwake ni mzaha – utajiri huo wake hauwezi hata kidogo kulinganishwa na mifugo wake.

Muhoozi alihoji ni kwa nini hajapata jibu kutoka kwa Jay-Z, wiki chache baada ya kumtaka kukubali pambano ambalo lingeona mshindi kati yao akimchukua Beyonce kama mke wake – bila kujali kwamba Beyonce tayari ni mke halali wa bilionea Jay-Z.

Alisema kwamba ikiwa Jay-Z hatatoa tamko, huenda akapendelea kupanga njama ya kumteka nyara Beyonce na kumchukua kwa nguvu kutoka kwa Jay-Z.

“Nimesubiri kwa wiki moja sasa. Hakuna jibu kutoka kwa Jay-Z? Je, niende tu kumkamata huyo mwanamke? Eti Jay-Z ni bilionea? Huo ni utani! Ng'ombe wangu wana thamani kuliko yeye!” Muhoozi alihoji.

Mwanajeshi huyo ambaye ameonekana kudata katika penzi la Beyonce – mama wa Watoto 3 ambaye amedumu kwa ndoa na Jay-Z tangu 2008 – alisema kwamba wazo la kumkamata kwa nguvu likishindikana, atakusanya kura ya maoni kuona wangapi wanamuunga mkono kwamba Beyonce anafaa kuwa wa kwake na wala si wa Jay-Z.

Pia alisema kwamba tangu aanzishe vuguvugu la kumtaka Beyonce kumwacha Jay-Z na kuja kwake, amepokea mialiko kadhaa kutoka kwa vyombo vya Habari Marekani vikimtaka kulizungumzia hilo moja kwa moja kwenye kamera.

“Waafrika na Waasia wangapi wananiunga mkono katika kumwokoa Beyonce kutoka kwa Jay-Z? Retweet na like. Baadhi ya Chaneli za Habari za Marekani zimeniomba nije kueleza jinsi Beyonce ni mke wangu, niko tayari kuja...” Muhoozi Kainerugaba alisema.

Lakini je, ni kweli kwamba utajiri wa ng’ombe wa mwanawe Museveni unazidi maradufu utajiri wa msanii Jay-Z kutoka Marekani?

Kwa mujibu wa ripoti ya Forbes ya mwaka 2024, Jay-Z ndiye msanii Tajiri zaidi duniani akiongoza kwa utajiri wa dola bilioni 2.5 – sawa na shilingi bilioni 323 za Kenya.

Kazi kwako Jenerali Muhoozi Kainerugaba!

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved