logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afisa wa mazingira kaunti ya Nairobi atoa onyo kali baada ya mchuuzi kumuumiza kanjo

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mosiria alisimulia jinsi afisa wa kanjo wa kike alivyoshambuliwa na mtu anayedaiwa kuwa mchuuzi katika moja ya mitaa ya katikati ya Nairobi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani23 April 2025 - 10:29

Muhtasari


  • Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mosiria alisimulia jinsi afisa wa kanjo wa kike alivyoshambuliwa na mtu anayedaiwa kuwa mchuuzi katika moja ya mitaa ya katikati ya Nairobi.
  • Afisa huyo wa mazingira aliapa kwamba uongozi mzima wa kaunti utahakikisha mchuuzi aliyetekeleza kitendo hicho kwa mwenzao anachukuliwa hatua madhubuti.

Geoffrey Mosiria, afisa wa mazingira kaunti ya Nairobi//FACEBOOK

AFISA anayesimamia usafi wa mazingira katika kaunti ya Nairobi, Geoffrey Mosiria ametoa onyo kali kwa hulka ya wachuuzi kuwashambulia na kuwaumiza maafisa wa kaunti maarufu kama kanjo, baada ya mmoja wao kushambuliwa.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mosiria alisimulia jinsi afisa wa kanjo wa kike alivyoshambuliwa na mtu anayedaiwa kuwa mchuuzi katika moja ya mitaa ya katikati ya Nairobi.

“Ni jambo la kusikitisha sana na halikubaliki kabisa kwamba mchuuzi alichagua kumshambulia afisa wa kaunti (mwanamke Askari wa kaunti) ambaye alikuwa akitekeleza majukumu yake halali akiwaomba waondoke kwenye njia ya umma ili kuruhusu watembea kwa miguu bila malipo. Hiki ni kitendo cha kutokujali cha hali ya juu, na hatutaruhusu kiende bila kuadhibiwa. Hatutaogopa. Utaratibu lazima udumishwe, na utawala wa sheria lazima itawala,” Mosiria alitema cheche.

Kwa mujibu wa Mosiria, wachuuzi huwa hawalipi kodi yoyote kwa serikali ya kaunti ya Nairobi na waliruhusiwa kuendesha biashara zao katika Maeneo waliyotengewa kwa hisani ya gavana lakini sasa wameanza kutumia vibaya ruhusa hiyo.

 “Wachuuzi jijini Nairobi hawalipi ada yoyote kwa serikali ya kaunti. Kwa nia njema, Mheshimiwa Gavana amewaruhusu kufanya kazi kutoka kwa njia maalum za nyuma ili kukuza fursa jumuishi za kiuchumi. Hata hivyo, wengine sasa wanatumia vibaya fursa hii kwa kuvamia njia za kupita miguu, kuzuia watembea kwa miguu, na mbaya zaidi kutumia vurugu wanapotakiwa kuzingatia sheria,” alifafanua.

Afisa huyo wa mazingira aliapa kwamba uongozi mzima wa kaunti utahakikisha mchuuzi aliyetekeleza kitendo hicho kwa mwenzao anachukuliwa hatua madhubuti.

Kanjo aliyeshambuliwa na mchuuzi Nairobi//Facebook- Geoffrey Mosiria KE

“Ifahamike wazi: afisa huyu ni binti wa mtu, mama wa mtu, na mtumishi wa umma aliyejitolea kutumikia watu wa Nairobi. Shambulio lolote dhidi ya afisa mmoja wa kaunti ni shambulio dhidi ya wafanyikazi wote wa kaunti, na tutajibu kwa uthabiti.”

“Hatutavumilia uasi. Watu waliohusika katika shambulio hili watatambuliwa, kukamatwa, na kufunguliwa mashtaka kwa kiwango kamili cha sheria. Pia tunakagua itifaki za utekelezaji ili kuhakikisha usalama na utu wa maafisa wetu wote wanaosonga mbele,” aliapa.

Katika siku za nyuma, vilio vilivyokuwepo ni vya maafisa wa kaunti kushambulia wachuuzi na hata kuharibu mtaji wao.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved