logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akothee awatahadharisha wanaume dhidi ya kumtongoza mitandaoni

Mama huyo wa watoto watano amewka wazi kuwa anapendelea kukutana na mtu ana kwa ana.

image
na Radio Jambo

Makala23 August 2022 - 10:33

Muhtasari


•Akothee ameweka wazi kuwa hawezi  kuanguka kwenye mtego wa mapenzi ya mitandaoni kwa kuwa anapendelea kukutana na mtu ana kwa ana.

•Kutokana na uwongo mwingi kwenye mitandao ya kijamii, Akothee amewaonya watoto wake dhidi ya kutangamana na watu mtandaoni.

Mwanamuziki mashuhuri Esther Akoth almaarufu Akothee amewataka wanaume kujiepusha kumtumia  jumbe tamu za kimahaba kwenye mitandao kwa nia kumtongoza.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mama huyo wa watoto watano ameweka wazi kuwa hawezi  kuanguka kwenye mtego wa mapenzi ya mitandaoni kwa kuwa anapendelea kukutana na mtu ana kwa ana.

"Nashangaa jinsi watu wanavyopata mapenzi kwa kuchumbiana mtandaoni , nashangaa ningewezaje kuteleza kwenye Dm ya mtu na kutarajia itokee🤔, ninaogopa sana wanaume wanaoandamana na kulamba midomo yao 24/7. Ninapendelea kukutana na mtu wangu katika maisha halisi na mduara ambapo ninaweza kufuatilia historia yake. Unaweza hata kukutana na kifo chako kwa jina la mapenzi," Akothee alisema.

Mwimbaji huyo amedokeza kuwa hofu yake ya mambo ya mitandaoni imetokana na matukio ya nyuma yaliyoishia kuuvunja moyo wake.

Amedai kuwa yeye ni mwathiriwa wa unafiki ulio kwenye mitandao ya kijamii kwani amewahi kukutana na watu wengi bandia pale.

"Na moyo wangu mjinga, nimeamini maneno ya mashabiki, wengine walinasa moyo wangu na nikaamua kuwasaidia, ikawa deni. Niliwaalika wengine kwa likizo na wakageuka kuwa wa kunichukia, wengine waliomba kukutana nami na kutangaza jinsi wanavyonipenda, ili tu kuzima ubaya wao na kunigeuza kuwa mwathirika wa sumu yao," Akothee alifunguka.

Kutokana na uwongo mwingi kwenye mitandao ya kijamii, Akothee amewaonya watoto wake dhidi ya kutangamana na watu mtandaoni.

"Acha hata kuchumbiana, hata kuwa marafiki tu!" Alisema.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 42 ana watoto watano ambao wote wana kurasa za mitandao ya kijamii.

Binti zake watatu ni wakubwa na inaaminika kuwa wanasimamia akaunti zao wenyewe ilhali wanawe wawili ni wadogo na haijulikani wazi ni nani anayesimamia akaunti zao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved