logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mke amcheka mume wa zamani kwa kukopa benki kufadhili harusi yao iliyovunjika

Mke huyo ambaye alisema kwa madaha kwamba tayari ameshasonga mbele na maisha ya kupata mwenzi mpya, alimkejeli Ex wake kwa kubaki na deni la benki pamoja na riba

image
na MOSES SAGWEjournalist

Dakia-udaku24 March 2025 - 11:49

Muhtasari


  • “Ile shughuli ilikuwa ghali sana na sasa amebaki akilipia madeni peke yake wakati mimi niko vizuri katika maisha yangu ya kibiashara na pia nina mchumba mpya,” alisema.

Kuvunjika moyo

MWANAMKE wa Kenya anayeitwa amezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii baada ya kumkejeli aliyekuwa mume wake, ambaye alichukua mkopo kufadhili harusi yao ya kitamaduni.

Kulingana na mwanamke huyo aliyetalikiwa, mume wake wa zamani alitumia mkopo wa benki kulipia kila kitu wakati wa harusi yao ya kitamaduni ya kupendeza, lakini ndoa yao ilidumu kwa mwaka mmoja tu.

Akionekana kumfuma mkuki mume wake wa zamani kwa kile kilichoonekana kama uamuzi mbaya wa kifedha, alisema kwamba ndoa hiyo ilivunjika na mume huyo kubaki akilipia deni la mkopo.

Mke huyo ambaye alisema kwa madaha kwamba tayari ameshasonga mbele na maisha ya kupata mwenzi mpya, alimkejeli Ex wake kwa kubaki na deni la benki pamoja na riba lakini pia kuuguza moyo kutokana na ndoa kusambaratika.

“Kiwango [cha harusi] kilikuwa cha chini lakini mimi sikulipia hata senti kwa ruracio yangu. Yeye alilipia kila kitu kutoka kwa mavazi yangu, mapambo, mshereheshaji, video, chakula na hata vipodozi vyotealoigharamika yeye.”

“Ile shughuli ilikuwa ghali sana na sasa amebaki akilipia madeni peke yake wakati mimi niko vizuri katika maisha yangu ya kibiashara na pia nina mchumba mpya,” alisema.

caption

Mwanamke huyo alifuta chapisho lake baada ya kukosolewa vikali na watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao walikutana na dhihaka zake dhidi ya mumewe wa zamani.

Waliokatishwa tamaa zaidi wamemwita mwanamke asiye na shukrani. Wamependekeza hata alikuwa akisaliti penzi la mumewe walipokuwa bado kwenye ndoa.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved