logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilienda kwa Harmonize nikamkuta na boxer na Paula anampapasa kifuani - Mwijaku

Siku moja nilienda kwa Harmonize nikamkuta sebuleni amekaa na Boxer halafu Paula anampapasa kifuani mimi kama Mzazi sikupenda - Mwijaku.

image
na Radio Jambo

Makala12 October 2022 - 07:20

Muhtasari


• Nikamwambia hii sio sawa akaniambia haya ni mambo ya kifamilia yaache, akasema Pesa inaoongea - Mwijaku.

Mwijaku aibuka na jipya kuhusu Mahusiano ya Kajala bintiye Paula na Harmonize

Mtangazaji Mwijaku amezidi kumchimba mikwara msanii Harmonize kwa tuhuma za kutoka kimapenzi na Kajala Masanja pamoja na bintiye Paula Kajala kwa zamu.

Mwijaku alichukua hatua zaidi na kuenda mpaka kituo cha ustawi wa jamii kumshtaki Harmonize akitaka achukuliwe hatua za kisheria kwa kile alisema kwamba anamdhulumu Paula ambaye ni mtoto.

Kulingana na Mwijaku, Paula ni mtoto mdogo na anachopitia mikononi mwa Harmonize ni dhuluma za kimapenzi ambapo Harmonize anawatumia wote binti na mama kimapenzi.

Mwijaku alielezea kwamba Kajala mwenyewe amenyamazia suala hilo la Harmonzie kumtumia bintiye pia kimapenzi kutokana na ugumu na changamoto za kifedha ambazo zinawafanya wawili hao kuridhia kulala pamoja na msanii Harmonize.

Mtangazaji huyo hata alizidi kuelezea kwamba ana ushahidi mtupu wa kile alichokuwa akisema na kusimulia kuwa kwa wakati mmoja alitembelea familia hiyo na kuona jinsi Harmonize alivyokuwa anamfanyia Paula kutokana na ugumu wake wa kifedha.

Siku moja nilienda kwa Harmonize nikamkuta sebuleni amekaa na Boxer halafu Paula anampapasa kifuani mimi kama Mzazi sikupenda nikamwambia hii sio sawa akaniambia haya ni mambo ya kifamilia yaache, akasema Pesa inaoongea,” Mwijaku alisema.

Mwijaku alisema kuwa ni dhambi kubwa kwa Harmonize kutumia kigezo cha kuwa na pesa kwa kuwadhulumu Kajala na bintiye kimapenzi.

Awali mtangazaji huyo aliibua madai kwamba duka la nguo la Paula alimfungulia yeye na ndio maana amemrudisha kimawasiliano na hata kumfanya Paula kumkubali kama baba yake wa kambo, kinyume na awali amabpo binti huyo wa Kajala alikuwa hampendi kabisa Harmonize kutokana na sakata la awali la kumtumia picha za utupu wake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved