logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bahati na Diana B waenda likizo ughaibuni

Msanii Bahati na mkewe Diana B siku ya Jumatatu walifunga safari kwa ughaibuni.

image
na

Makala14 March 2023 - 05:09

Muhtasari


•Bahati alidai kuwa Diana alilalamika kuwa hakumfanyia lolote siku ya akina mama duniani hivyo basi aliamua kupeleka likizoni.

Msanii Bahati na mkewe Diana B siku ya Jumatatu walifunga safari kuelekea kwenye likizo ughaibuni.

Kwenye mtandao wa Instagram, Bahati na Diana walionekana  wakiabiri ndege  katika uwanja wa ndege wa JKIA. Wawili hao walijiburudisha kwa vyakula vya kumezewa mate na kulishana mahaba si haba.Waliipamba kuondoka kwao kwa kuvaa nguo zinazolingana.

 

Bahati na Diana walisema kuwa  siku zijazo wakiwa kwenye likizo ndizo zitakuwa siku bora zaidi kwa kumbukumbu, pia aliuliza mashabiki ni kipi atamfanyia Diana B ili iwe kumbukumbu bora zaidi kwake.

"Mpenzi, siku chache zinazofuata zitakuwa bora zaidi kiliko ambazo umekuwa nazo,kumbukumbu, Nimfanyie nini mrembo huyu ili iwe likizo bora zaidi?" Bahati aliuliza.

 

Bahati alidai kuwa Diana alilalamika kuwa hakumfanyia lolote siku ya akina mama duniani hivyo basi aliamua kumpeleka likizoni.Ingawa hakusema ni wapi wanakokwenda,walionekana kwenye sehemu ya ndege za Turkish Airlines.

"Malkia wangu alilalamika kuwa sikumfanyia lolote siku ya wanawake," alisema Bahahati.Aliongeza kwa kuuliza kama watu wanajua wanakoenda

Diana B kwenye mtandao wa Instagram aliuliza ni kwa nini Bahati hakumweka mtandaoni siku ya wanawake duniani.

"Bahati kwanini hukunipost siku ya wanawake duniani?" Diana alichapisha

Diana alifurahia safari yake na Diana mtandaoni,

"Kusafiri duniani na mpenzi wangu Bahati,' Diana alisema.

Diana B hivi majuzi amekuwa na ugomvi mtandoni baada ya kudai kuwa Andrew Kibe anatusi watu mtandaoni ilhali yeye ni masikini.Andrew Kibe kwa upande wake alijibu akisema kuwa Diana hajaona gari lake alilonunua  hapo awali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved