logo

NOW ON AIR

Listen in Live

RIP: Promota na Meneja wa zamani wa Aslay afariki dunia!

"Hukua BOSS tu kwetu,ulikua BABA kwenye shida na kwenye raha" - Stamina aliomboleza.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 March 2023 - 11:09

Muhtasari


• “Babaz shukrani kwa mema yote, lala salama kiongozi,” Aslay alimuomboleza.

Aslay na wasanii wengine wakiwa na Babaz kipindi cha uhai wake.

Mdau wa muziki wa kizazi kipya kutoka ukanda wa pwani ya Kenya Mussa Babaz amefariki dunia.

Wengi wanamtambua Babaz kwa mchango wake mkubwa katika kukuza na kuwashika mkono vijana wengi waliokuwa wanaimba muziki wa Bongo Fleva hasa kutoka nchini Kenya na Tanzania pia kwa kiasi kikubwa.

Taarifa za kifo chake zilivujishwa mitandaoni na mtangazaji Mzazi Willy Tuva ambaye kwa kushirikiana na wasanii wengine wengi walimuomboleza Babaz kama mtu aliyejitolea pakubwa katika kukuza vipaji vya uimbaji katika mataifa haya mawili.

Una mchango mkubwa sana katika tasnia ya burudani. Umewashika mkono wasanii wengi tajika. Umekuwa rafiki na ndugu yangu. Tumekuwa familia moja. Tumefaana kwa mengi. Leo umetutoka na kutuachia majonzi makubwa. Nitabaki na kumbukumbu njema za wema wako. Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un,” Mtangazaji huyo aliandika.

Babaz enzi za uhai wake, aliwahi fanya kazi ya kuwasimamia wasanii wa kufoka kama Stamina na Roma Mkatoliki kutoka kundi la Rostam, akafanya kazi na Aslay, Chege Chigunda, Jay Melody miongoni mwa wengine wengi.

“Babaz shukrani kwa mema yote, lala salama kiongozi,” Aslay alimuomboleza.

Nikisema niandike nitaandika vitu vingi sana,ila tu niseme imeniumiza mimi pamoja na familia yetu nzima ya ROSTAM!! Hukua BOSS tu kwetu,ulikua BABA kwenye shida na kwenye raha!! PUMZIKA KWA AMANI BABA YETU MUSSA BABAZ WA BABAZ😭 Ile simu ya juzi tunamtania @roma_zimbabwe ndio ilikua unaniaga kumbe!!daah nimeumia kwa kweli...” Stamina aliandika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved