logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Treni iliyokuwa imepeleka mafuta ya petroli Nanyuki yashika moto

Waliokuwa ndani ya treni hiyo ya mabehewa sita waliweza kujinusuru na kuanza kujaribu kuthibiti moto huo kabla ya kuenea sana.

image
na Radio Jambo

Habari06 June 2021 - 20:52

Muhtasari


•Mwakani 2011, treni lililokuwa limebeba abiria zaidi ya 1000 lilishika moto katika maeneo ya Kibra . Kiini cha moto huo pia kilisemekana kuwa matatizo ya stima.

Gari moshi

Gari moshi lililokuwa limepeleka mafuta ya petroli Nanyuki lilishika moto katika lilipokuwa kwenye safari ya kurudi Nairobi siku ya Jumapili.

Tukio hilo ambalo lilifanyika mida ya saa tatu unusu lilithibitiwa na wazima moto kutoka Murang'a baada ya kipindi kifupi.

Shirika la Kenya Railways(KR) limeripoti kuwa moto huo ulisababishwa na kasoro ya stima.

"Tukio hilo liliripotiwa mara hiyo na wahandisi wa KR wakatumwa katika maeneo yale ili kuchunguza kilichosababisha moto ule. Wazima moto kutoka Murang'a walikuwa pale ili kuthibiti moto ule" shirika la KR lilitangaza.Hata hivyo, hakuna majeruhi wowote walioripotiwa pale.

Waliokuwa ndani ya treni hiyo ya mabehewa sita waliweza kujinusuru na kuanza kujaribu kuthibiti moto huo kabla ya kuenea sana.

Kenya Railways wameripoti kuwa safari za gari moshi hilo zimesitishwa kama tahadhari tu kuona kuwa lingesababisha madhara kubwa sana siku ya Jumapili.

"Kwa wakati huo, injini nyingine ilitumwa kutoka Nairobi ili kuhakikisha magari hayo ya mizigo yalifika salama katika karakana za Nairobi Central" shirika la KR lilieleza.

Mwakani 2011, treni lililokuwa limebeba abiria zaidi ya 1000 lilishika moto katika maeneo ya Kibra . Kiini cha moto huo kilisemekana kuwa matatizo ya stima pia. 

Abiria wote waliweza kunusurika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved