logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanadada anayedai kuwa mpango wa kando wa spika Lusaka adai kulipwa milioni 25

Anamtaka Lusaka kugharamia mahitaji ya mtoto ambaye amebeba.

image
na Radio Jambo

Burudani22 June 2021 - 02:54

Muhtasari


• Anataka mahakama kumlazimisha spika kuwa anampatia Sh200,000 kila mwezi  za kukimu mahitaji ya mtoto huyo ambaye hajazaliwa bado

•Alidai kuwa amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanasiasa huyo aliyekuwa gavana wa Bungoma kwa kipindi cha miaka mitatu na kutokana na uhusiano huo akapata mimba

Spika wa seneti Kenneth Lusaka

Mwanamke aliyedai kuwa mpango wa kando wa spika wa seneti Kenneth Lusaka anataka shilingi milioni 25 kutoka kwake ili kugharamia mahitaji ya mtoto ambaye amebeba.

Mwanamke huyo ambaye alifika mahakamani siku ya Jumatatu na kudai kuwa mimba aliyokuwa amebeba ni ya Lusaka anataka mahakama kumlazimisha spika kuwa anampatia Sh200,000 kila mwezi  za kukimu mahitaji ya mtoto huyo ambaye hajazaliwa bado

Alidai kuwa amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanasiasa huyo aliyekuwa gavana wa Bungoma kwa kipindi cha miaka mitatu na kutokana na uhusiano huo akapata mimba.

Wakili wa mlalamishi, Danstan Omari ameomba mahakama kuagiza Lusaka kukubali majukumu ya mtoto huyo. Alimtaka spika kugharamia bili zote za kliniki na hospitali katika ujauzito wa mlalamishi.

Mlalamishi alisema kuwa Lusaka alikuwa amekanusha uhusiano wowote na mimba ambayo alikuwa amebeba licha ya kujua kuwa walikuwa wakishiriki tendo la ndoa bila kinga.

Jaji James Makau alifanya dharura kesi hiyo siku ya Jumatatu na kuagiza isikizwe mnamo Julai 7.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved