logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hofu baada ya mwanafunzi wa KMTC kupatikana ameuliwa kinyama hostelini Homa Bay

Polisi wanamuwinda mpenzi wa marehemu ambaye kwa sasa hapatikani na amezima simu yake.

image
na Radio Jambo

Burudani06 July 2021 - 03:31

Muhtasari


•Mwili wa Emily Chepkemoi, 23, ulipatikana juu ya kitanda kilichokuwa ndani ya hosteli yake  huku umezingirwa na dimbwi la damu.

•Inatuhumiwa kuwa mpenziwe Chepkemoi ndiye alitekeleza unyama huo usiku wa Ijumaa.

Wanafunzi wa KMTC Homa Bay wamuomboleza mmoja wao aliyepatikana ameuliwa Jumapili

Hali ya mshtuko  na hofu imetanda katika chuo cha kufundisha masomo ya udaktari mjini Homabay (KMTC-Homabay Town)  baada ya mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kupatikana ameuliwa siku ya Jumapili.

Mwili wa Emily Chepkemoi, 23, ulipatikana juu ya kitanda kilichokuwa ndani ya hosteli yake  huku umezingirwa na dimbwi la damu.

Majirani ambao walinusa harufu kali kutoka ndani ya chumba hicho waliamua kuvunja mlango na ndipo wakakumbana na mwili wa Emily ambaye alikuwa ameuliwa kinyama kisha wakaarifu maafisa wa polisi. 

Mwili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Homa Bay Teaching and Referral huku upasuaji wa mwili ukisubiriwa.

Ingawa haijabainika wazi aliyetelekeza kitendo hicho na kwa nini, polisi wanamuwinda mpenzi wa marehemu ambaye kwa sasa hapatikani na amezima simu yake.

Chifu msaidizi wa  mji wa Homabay, Duncan Okech alisema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa amedungwa kwa kisu mara mbili kwenye kichwa na shingo.

Inatuhumiwa kuwa mpenziwe Chepkemoi ndiye alitekeleza unyama huo usiku wa Ijumaa.

Kiongozi wa muungano wa wanafunzi katika chuo hicho, David Odhiambo aliagiza haki kutendeka na akaomba uchunguzi kamilifu kufanyika.

"Wanafunzi wengi walipatwa na mshangao na hawakuhudhuria madarasa yao kufuatia tukio hilo. Tunamuomboleza mmoja wetu na tunataka haki itendeke" Odhiambo alisema Jumatatu.

Maafisa wa DCI  walisema kuwa wanafuata miongozo muhimu ambayo wana matumaini itawaongoza waweze kutia mbaroni washukiwa wa mauaji hayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved