logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msichana 16, akamatwa kwa kumuua binamuye, Siaya

Naibu Chifu aliripoti kwa polisi tukio la mauaji katika kijiji cha Nyandiwa.

image
na

Habari07 March 2024 - 07:41

Muhtasari


• Mshukiwa ambaye ni mgonjwa wa akili alikuwa akicheza ndani ya boma lao na watoto wengine wadogo.

 

Polisi katika Kaunti ya Siaya wanachunguza kisa ambapo msichana mwenye umri wa miaka 16 anadaiwa kumuua mpwawe wa umri wa miaka 9 kwa kutumia mkuki katika kijiji cha Nyandiwa katika kaunti ndogo ya Alego/Usonga.

Naibu Chifu wa Nyandiwa Joseph Otieno Aloo aliripoti kwa Kituo cha Polisi cha Siaya kwamba kulikuwa na tukio la mauaji katika kijiji cha Nyandiwa.

Kulingana na Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Siaya Cleti Kimaiyo, maafisa kutoka Kituo cha Polisi cha Siaya walifika eneo la tukio na kubaini kuwa mshukiwa ambaye ni mgonjwa wa akili alikuwa akicheza ndani ya boma lao na watoto wengine wadogo.

Alieleza kuwa ghafla kulitokea kutoelewana kati yao kabla ya mtuhumiwa kuingia nyumbani kwa baba yake na kuchukuwa mkuki ambao aliwarushia watoto wengine na kumdunga kichwani mtoto wa miaka tisa ambaye alikufa papo hapo.

Akithibitisha kisa hicho, Bw. Kimaiyo alisema eneo la tukio lilishughulikiwa na kurekodiwa kabla ya mwili huo kuhamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Siaya huku uchunguzi kuhusu kisa hicho ukiendelea.

Mshukiwa alikamatwa na anasaidia polisi katika uchunguzi. Silaha ya mauaji pia ilipatikana na kuwekwa kama ushahidi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved